Ahmad (Rahimahu Allaah), Abu Daawuud (Rahimahu Allaah) na an-Nasaa’iy (Rahimahu Allaah) wamepokea kupitia kwa Abu Dharr (Radhiya Allaahu ´anh), ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah haachi kumgeukia mja wakati wa kuswali kwake muda wa kuwa hajageuka. Akigeuka humwondokea.”[1]
Imaam Ahmad na at-Tirmidhiy wamepokea kupitia kwa al-Haarith al-Ash´ariy (Radhiya Allaahu ´anh), ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah alimwamrisha Yahyaa bin Zakariyyaa mambo matano… Nakuamrisheni swalah. Allaah huweka uso Wake mbele ya uso wa mja Wake muda wa kuwa hajageuka.”[2]
Zipo Hadiyth zingine nyingi zenye maana kama hiyo.
`Atwaa’ amesimulia kuwa alimsikia Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anh) akisema:
“Anaposwali mmoja wenu basi asigeuke, kwani anamnong´oneza Mola wake. Mola wake yuko mbele yake na yeye anamnong´oneza. Hivyo basi asigeuke.”
`Atwaa’ (Rahimahu Allaah) amesema:
“Tumefikiwa na khabari kwamba Mola (‘Azza wa Jall) anasema: “Ee Mwanadamu! Unamgeukia kwa faida gani? Mimi ni bora kwako kuliko yule unayemgeukia.”
al-Bazzaar na wengine wamepokea kwa njia ya masimulizi ya kinabii. Hata hivyo Swahiyh zaidi ni kwamba ni masimulizi ya Swahabah.
Abu ´Imraan al-Juuniy (Rahimahu Allaah) amesema:
“Allaah (‘Azza wa Jall) alimteremshia wahy Muusa (‘alayhis-Salaam): “Ee Muusa! Unaposimama mbele Yangu, basi simama kama mja masikini na mtwevu. Jilaumu nafsi yako, kwa sababu ina haki zaidi ya kulaumiwa. Ninong´oneze kwa moyo wenye aibu na ulimi wa kweli.”[3]
[1] Ahmad (5/172), Abu Daawuud (909) na an-Nasaa’iy (1195). Swahiyh kwa mujibu wa Ibn Khuzaymah (1/244) na al-Haakim (1/361). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Dhwa´iyf Sunan Abiy Daawuud” (909).
[2] Ahmad (5/849-850) na at-Tirmidhiy (2863), ambaye amesema kuwa Hadiyth ni nzuri, Swahiyh na ngeni. Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh Sunan at-Tirmidhiy” (2863).
[3] Hilyat-ul-Awliyaa’ (5/66).
- Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn ´Abdur-Rahmaan bin Rajab al-Hanbaliy (afk. 795)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Khushuu´ fiys-Swalaah, uk. 72-74
- Imechapishwa: 24/11/2025
Ahmad (Rahimahu Allaah), Abu Daawuud (Rahimahu Allaah) na an-Nasaa’iy (Rahimahu Allaah) wamepokea kupitia kwa Abu Dharr (Radhiya Allaahu ´anh), ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah haachi kumgeukia mja wakati wa kuswali kwake muda wa kuwa hajageuka. Akigeuka humwondokea.”[1]
Imaam Ahmad na at-Tirmidhiy wamepokea kupitia kwa al-Haarith al-Ash´ariy (Radhiya Allaahu ´anh), ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah alimwamrisha Yahyaa bin Zakariyyaa mambo matano… Nakuamrisheni swalah. Allaah huweka uso Wake mbele ya uso wa mja Wake muda wa kuwa hajageuka.”[2]
Zipo Hadiyth zingine nyingi zenye maana kama hiyo.
`Atwaa’ amesimulia kuwa alimsikia Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anh) akisema:
“Anaposwali mmoja wenu basi asigeuke, kwani anamnong´oneza Mola wake. Mola wake yuko mbele yake na yeye anamnong´oneza. Hivyo basi asigeuke.”
`Atwaa’ (Rahimahu Allaah) amesema:
“Tumefikiwa na khabari kwamba Mola (‘Azza wa Jall) anasema: “Ee Mwanadamu! Unamgeukia kwa faida gani? Mimi ni bora kwako kuliko yule unayemgeukia.”
al-Bazzaar na wengine wamepokea kwa njia ya masimulizi ya kinabii. Hata hivyo Swahiyh zaidi ni kwamba ni masimulizi ya Swahabah.
Abu ´Imraan al-Juuniy (Rahimahu Allaah) amesema:
“Allaah (‘Azza wa Jall) alimteremshia wahy Muusa (‘alayhis-Salaam): “Ee Muusa! Unaposimama mbele Yangu, basi simama kama mja masikini na mtwevu. Jilaumu nafsi yako, kwa sababu ina haki zaidi ya kulaumiwa. Ninong´oneze kwa moyo wenye aibu na ulimi wa kweli.”[3]
[1] Ahmad (5/172), Abu Daawuud (909) na an-Nasaa’iy (1195). Swahiyh kwa mujibu wa Ibn Khuzaymah (1/244) na al-Haakim (1/361). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Dhwa´iyf Sunan Abiy Daawuud” (909).
[2] Ahmad (5/849-850) na at-Tirmidhiy (2863), ambaye amesema kuwa Hadiyth ni nzuri, Swahiyh na ngeni. Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh Sunan at-Tirmidhiy” (2863).
[3] Hilyat-ul-Awliyaa’ (5/66).
Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn ´Abdur-Rahmaan bin Rajab al-Hanbaliy (afk. 795)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Khushuu´ fiys-Swalaah, uk. 72-74
Imechapishwa: 24/11/2025
https://firqatunnajia.com/17-makatazo-ya-kugeukageuka-wakati-wa-swalah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
