Hata hivyo imethibiti kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba hakuna yeyote atakayemuona Allaah mpaka atakapokufa[1]. Wala hakuna dalili iliyothibiti inayojulisha kuwa yeye pia (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimuona. Bali kumethibiti kinyume chake. Abu Dharr (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
”Ee Mtume wa Allaah! Je, ulimuona Mola wako?” Akajibu: ”Ni Nuru. Nitamuonaje?”[2]
Isitoshe ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amelikanusha hilo[3], jambo ambalo ndio msingi na hivyo ndilo linalotakiwa kushikiliwa.
[1] Muslim.
[2] Muslim (178).
[3] al-Bukhaariy (4855) na Muslim (177).
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah – Sharh wa Ta´liyq, uk. 30
- Imechapishwa: 18/09/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)