[1] Inajuzu kwake kutoka kwa ajili ya kutekeleza dharura fulani au kutoa kichwa chake nje ya msikiti ili kioshwe na kichanuliwe. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akinitolea kichwa chake wakati anafanya I´tikaaf msikitini na mimi niko chumbani mwangu. Nikamtana [na katika upokezi mwingine: nikamuosha nikiwa katika hedhi yangu na hakuna kilichokuwa kikitutenganisha mimi na yeye isipokuwa tu kizingiti cha mlango] na pindi alipokuwa anafanya I´tikaaf alikuwa haingii nyumbani isipokuwa kwa sababu ya dharura fulani.”[1]
[2] Inajuzu kwa mwenye kufanya I´tikaaf na mwengineo kutawadha msikitini. Mwanamume aliyekuwa anamfanyia kazi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alitawadha msikitini wudhuu´ khafifu.”[2]
[3] Vilevile inafaa kwake kusimamisha hema dogo nyuma ya msikiti akawa anafanya I´tikaaf ndani yake. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) kwa amri ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimsimamishia Khibaa´[3] pindi (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapofanya I´tikaaf[4].
Vilevile kuna wakati alifanya I´tikaaf kwenye kuba dogo ambayo mlango wake ulikuwa umefanywa kwa mkeka.
[1] Ameipokea al-Bukhaariy, Muslim, Ibn Abiy Shaybah na Ahmad na nyongeza ya kwanza ni ya kwao wawili. Imetajwa katika “Swahiyh Abiy Daawuud” (2131-2132).
[2] Ameipokea al-Bayhaqiy kwa mlolongo wa wapokezi mzuri na Ahmad (05/364) kwa ufupi kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh.
[3] Khibaa´ ni kanyumba ka kiarabu kanakotokamana na manyoya au pamba, lakini sio nywele, na kamesimamishwa na nguzo mbili au tatu. (an-Nihaayah)
[4] Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim kutoka kwa ´Aaishah. Kitendo ni cha al-Bukhaariy na amri ni ya Muslim.
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qiyaam Ramadhwaan, uk. 37-39
- Imechapishwa: 07/05/2019
[1] Inajuzu kwake kutoka kwa ajili ya kutekeleza dharura fulani au kutoa kichwa chake nje ya msikiti ili kioshwe na kichanuliwe. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akinitolea kichwa chake wakati anafanya I´tikaaf msikitini na mimi niko chumbani mwangu. Nikamtana [na katika upokezi mwingine: nikamuosha nikiwa katika hedhi yangu na hakuna kilichokuwa kikitutenganisha mimi na yeye isipokuwa tu kizingiti cha mlango] na pindi alipokuwa anafanya I´tikaaf alikuwa haingii nyumbani isipokuwa kwa sababu ya dharura fulani.”[1]
[2] Inajuzu kwa mwenye kufanya I´tikaaf na mwengineo kutawadha msikitini. Mwanamume aliyekuwa anamfanyia kazi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alitawadha msikitini wudhuu´ khafifu.”[2]
[3] Vilevile inafaa kwake kusimamisha hema dogo nyuma ya msikiti akawa anafanya I´tikaaf ndani yake. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) kwa amri ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimsimamishia Khibaa´[3] pindi (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anapofanya I´tikaaf[4].
Vilevile kuna wakati alifanya I´tikaaf kwenye kuba dogo ambayo mlango wake ulikuwa umefanywa kwa mkeka.
[1] Ameipokea al-Bukhaariy, Muslim, Ibn Abiy Shaybah na Ahmad na nyongeza ya kwanza ni ya kwao wawili. Imetajwa katika “Swahiyh Abiy Daawuud” (2131-2132).
[2] Ameipokea al-Bayhaqiy kwa mlolongo wa wapokezi mzuri na Ahmad (05/364) kwa ufupi kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh.
[3] Khibaa´ ni kanyumba ka kiarabu kanakotokamana na manyoya au pamba, lakini sio nywele, na kamesimamishwa na nguzo mbili au tatu. (an-Nihaayah)
[4] Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim kutoka kwa ´Aaishah. Kitendo ni cha al-Bukhaariy na amri ni ya Muslim.
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qiyaam Ramadhwaan, uk. 37-39
Imechapishwa: 07/05/2019
https://firqatunnajia.com/16-ni-yepi-yanayojuzu-wakati-wa-itikaaf/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)