Hapa ni baadhi ya maneno ya maimamu juu ya maudhui haya:
1 – Imepokelewa kutoka kwa al-Hasan al-Baswriy amesema:
”Mutwarrif alizungumza maneno yasiyokuwa na kifani kuhusu suala hili. Wakasema: ”Umesema nini, ee Abu Sa´iyd?” Akasema: ”Himdi zote njema ni stahiki ya Ambaye katika kumuamini ni kujahili yale ambayo hakujisifu Mwenyewe.”
81 – al-Awzaa´iy amesema:
”az-Zuhriy na Mak-huul walikuwa wakisema: ”Zipitisheni Hadiyth hizi kama zilivyokuja pasi na kuzifanyia namna.”
Wawili hao ni miongoni mwa wanafunzi wakubwa wa Maswahabah. Upokezi huo ni Swahiyh.
82 – Imesihi kwamba al-Waliyd bin Muslim amesema:
”Nilimuuliza Maalik bin Anas, Sufyaan ath-Thawriy, al-Layth bin Sa´d na al-Awzaa´iy kuhusu Hadiyth kuhusu sifa. Wakasema: ”Zipitisheni kama zilivyokuja.”
Maalik alikuwa ni imamu wa Madiynah, ath-Thawriy alikuwa ni imamu wa Kuufah, al-Awzaa´iy alikuwa ni imamu wa Dameski na al-Layth alikuwa ni imamu wa Misri. Hawa ni miongoni mwa wanafunzi wa wanafunzi wa Maswahabah wakubwa.
83 – Muhammad bin al-Hasan – ambaye ni mwanachuoni wa ´Iraaq – amesimulia maafikiano juu ya suala hilo. al-Laalakaa´iiy amepokea kwa cheni ya wapokezi wake akasema:
”Wanazuoni Mashariki mpaka Magharibi wameafikiana juu ya kuamini Qur-aan na Sunnah zilizopokea wapokezi wenye kuaminika kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba zinatakiwa kuaminiwa kuhusu sifa za Mola (´Azza wa Jall) pasi na tafsiri, maelezo wala kufananisha. Yule mwenye kufasiri kitu katika hizo basi ametoka nje ya njia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akatengana na mkusanyiko. Hawakueleza wala kufasiri. Waliamini yale yaliyomo ndani ya Qur-aan na Sunnah na wakanyamaza. Yule mwenye kusema kama alivosema Jahm basi ametengana na mkusanyiko. Kwa sababu amemweleza kwa kisichokuwa kitu.
84 – Sufyaan bin ´Uyaynah amesema:
”Kila ambacho Allaah (Ta´ala) amejisifu Mwenyewe ndani ya Qur-aan basi kule kukisoma ndio tafsiri yake pasi na kufananisha wala kuyawekea namna.”
ash-Shaafi´iy amesema kuhusu huyu Sufyaan bin ´Uyaynah:
”Kama isingelikuwa yeye na Maalik, basi ingelipotea elimu ya Hijaaz.
85 – Aflah bin Muhammad amesema:
“Nilisema kumwambia Ibn-ul-Mubaarak: “Ee Abu ´Abdir-Rahmaan! Mimi nachukia kuzungumzia sifa za Mola.” Akasema: “Mimi ni mtu ambaye nachukia zaidi, lakini pindi Qur-aan inatamka kitu basi nasi tunakisema na pindi mapokezi yanapofikisha kitu basi tunakipokea.”
Baadhi ya maimamu wamesema:
”Ibn-ul-Mubaarak ni Kiongozi wa waumini katika kila kitu. Waislamu wameafikiana juu ya kuongoka kwake.”
- Muhusika: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 82-84
- Imechapishwa: 04/06/2024
Hapa ni baadhi ya maneno ya maimamu juu ya maudhui haya:
1 – Imepokelewa kutoka kwa al-Hasan al-Baswriy amesema:
”Mutwarrif alizungumza maneno yasiyokuwa na kifani kuhusu suala hili. Wakasema: ”Umesema nini, ee Abu Sa´iyd?” Akasema: ”Himdi zote njema ni stahiki ya Ambaye katika kumuamini ni kujahili yale ambayo hakujisifu Mwenyewe.”
81 – al-Awzaa´iy amesema:
”az-Zuhriy na Mak-huul walikuwa wakisema: ”Zipitisheni Hadiyth hizi kama zilivyokuja pasi na kuzifanyia namna.”
Wawili hao ni miongoni mwa wanafunzi wakubwa wa Maswahabah. Upokezi huo ni Swahiyh.
82 – Imesihi kwamba al-Waliyd bin Muslim amesema:
”Nilimuuliza Maalik bin Anas, Sufyaan ath-Thawriy, al-Layth bin Sa´d na al-Awzaa´iy kuhusu Hadiyth kuhusu sifa. Wakasema: ”Zipitisheni kama zilivyokuja.”
Maalik alikuwa ni imamu wa Madiynah, ath-Thawriy alikuwa ni imamu wa Kuufah, al-Awzaa´iy alikuwa ni imamu wa Dameski na al-Layth alikuwa ni imamu wa Misri. Hawa ni miongoni mwa wanafunzi wa wanafunzi wa Maswahabah wakubwa.
83 – Muhammad bin al-Hasan – ambaye ni mwanachuoni wa ´Iraaq – amesimulia maafikiano juu ya suala hilo. al-Laalakaa´iiy amepokea kwa cheni ya wapokezi wake akasema:
”Wanazuoni Mashariki mpaka Magharibi wameafikiana juu ya kuamini Qur-aan na Sunnah zilizopokea wapokezi wenye kuaminika kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba zinatakiwa kuaminiwa kuhusu sifa za Mola (´Azza wa Jall) pasi na tafsiri, maelezo wala kufananisha. Yule mwenye kufasiri kitu katika hizo basi ametoka nje ya njia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akatengana na mkusanyiko. Hawakueleza wala kufasiri. Waliamini yale yaliyomo ndani ya Qur-aan na Sunnah na wakanyamaza. Yule mwenye kusema kama alivosema Jahm basi ametengana na mkusanyiko. Kwa sababu amemweleza kwa kisichokuwa kitu.
84 – Sufyaan bin ´Uyaynah amesema:
”Kila ambacho Allaah (Ta´ala) amejisifu Mwenyewe ndani ya Qur-aan basi kule kukisoma ndio tafsiri yake pasi na kufananisha wala kuyawekea namna.”
ash-Shaafi´iy amesema kuhusu huyu Sufyaan bin ´Uyaynah:
”Kama isingelikuwa yeye na Maalik, basi ingelipotea elimu ya Hijaaz.
85 – Aflah bin Muhammad amesema:
“Nilisema kumwambia Ibn-ul-Mubaarak: “Ee Abu ´Abdir-Rahmaan! Mimi nachukia kuzungumzia sifa za Mola.” Akasema: “Mimi ni mtu ambaye nachukia zaidi, lakini pindi Qur-aan inatamka kitu basi nasi tunakisema na pindi mapokezi yanapofikisha kitu basi tunakipokea.”
Baadhi ya maimamu wamesema:
”Ibn-ul-Mubaarak ni Kiongozi wa waumini katika kila kitu. Waislamu wameafikiana juu ya kuongoka kwake.”
Muhusika: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 82-84
Imechapishwa: 04/06/2024
https://firqatunnajia.com/16-msimamo-wa-salaf-walioafikiana-juu-ya-sifa-za-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
