Wanazuoni (Rahimahumu Allaah) wamekhitilafiana kuhusu mtu aliyekula au kunywa hali ya kuwa amesahau na yeye ni mwenye kufunga juu ya mitazamo miwili tofauti:
1 – Halazimiki kulipa siku nyingine na swawm yake ni sahihi. Haya ndio madhehebu ya wanazuoni wengi katika Hanafiyyah[1], Shaafi’iyyah[2] na Hanaabilah[3], ambayo ndio maoni sahihi ambayo wanaonelea hivo kikosi kikubwa cha wanafunzi wa Maswahabah, maimamu, wanazuoni na wakaguzi[4].
2 – Anapaswa kulipa siku hiyo aliyokula. Haya ndio madhehebu ya Imaam Maalik[5] na Rabiy’ah bin ´Abdir-Rahmaan[6] (Rahimahumu Allaah). Huenda Imaam Maalik hakufikiwa na Hadiyth na hivyo hakuipokea katika ”al-Muwattwa’”. Kwa hiyo anakuwa ni mwenye kupewa udhuru.
Sahihi ni kama ilivyotangulia ya kwamba hatoilipa siku hiyo, jambo ambalo linathibitishwa na Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Allaah (´Azza wa Jall) anasema:
فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّـهِ وَالرَّسُولِ
“Mkizozana juu ya jambo, basi lirudisheni kwa Allaah na Mtume.”[7]
Hoja ipo katika maneno ya Allaah na maneno ya Mtume wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] Tazama ”al-Uswl-ul-Ma´ruuf bil-Mabsuutw” (02/201) ya ash-Shaybaaniy na ”al-Hujjah ´alaa Ahl-il-Madiynah (01/391).
[2] Tazama ”al-Umm” cha ash-Shaafi’iy (02/106) na ”al-Haawiy al-Kabiyr” (03/456).
[3] Tazama ”Masaa-il Imaam Ahmad wa Ishaaq Ibn Raahuuyah (03/1236) na al-Mughniy (03/131) ya Ibn Qudaamah.
[4] al-Istidhkaar (03/319) cha Ibn ´Abd-il-Barr.
[5] ”al-Muwattwa´” Malik (03/437) na ”al-Istidhkaar” (03/319) cha Ibn ´Abd-il-Barr.
[6] al-Istidhkaar (03/319) cha Ibn ´Abd-il-Barr.
[7] 04:59
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Taysiyr Dhil-In´am bisharh ´Umdat-il-Ahkaam (01/444)
- Imechapishwa: 02/03/2025
Wanazuoni (Rahimahumu Allaah) wamekhitilafiana kuhusu mtu aliyekula au kunywa hali ya kuwa amesahau na yeye ni mwenye kufunga juu ya mitazamo miwili tofauti:
1 – Halazimiki kulipa siku nyingine na swawm yake ni sahihi. Haya ndio madhehebu ya wanazuoni wengi katika Hanafiyyah[1], Shaafi’iyyah[2] na Hanaabilah[3], ambayo ndio maoni sahihi ambayo wanaonelea hivo kikosi kikubwa cha wanafunzi wa Maswahabah, maimamu, wanazuoni na wakaguzi[4].
2 – Anapaswa kulipa siku hiyo aliyokula. Haya ndio madhehebu ya Imaam Maalik[5] na Rabiy’ah bin ´Abdir-Rahmaan[6] (Rahimahumu Allaah). Huenda Imaam Maalik hakufikiwa na Hadiyth na hivyo hakuipokea katika ”al-Muwattwa’”. Kwa hiyo anakuwa ni mwenye kupewa udhuru.
Sahihi ni kama ilivyotangulia ya kwamba hatoilipa siku hiyo, jambo ambalo linathibitishwa na Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Allaah (´Azza wa Jall) anasema:
فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّـهِ وَالرَّسُولِ
“Mkizozana juu ya jambo, basi lirudisheni kwa Allaah na Mtume.”[7]
Hoja ipo katika maneno ya Allaah na maneno ya Mtume wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] Tazama ”al-Uswl-ul-Ma´ruuf bil-Mabsuutw” (02/201) ya ash-Shaybaaniy na ”al-Hujjah ´alaa Ahl-il-Madiynah (01/391).
[2] Tazama ”al-Umm” cha ash-Shaafi’iy (02/106) na ”al-Haawiy al-Kabiyr” (03/456).
[3] Tazama ”Masaa-il Imaam Ahmad wa Ishaaq Ibn Raahuuyah (03/1236) na al-Mughniy (03/131) ya Ibn Qudaamah.
[4] al-Istidhkaar (03/319) cha Ibn ´Abd-il-Barr.
[5] ”al-Muwattwa´” Malik (03/437) na ”al-Istidhkaar” (03/319) cha Ibn ´Abd-il-Barr.
[6] al-Istidhkaar (03/319) cha Ibn ´Abd-il-Barr.
[7] 04:59
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Taysiyr Dhil-In´am bisharh ´Umdat-il-Ahkaam (01/444)
Imechapishwa: 02/03/2025
https://firqatunnajia.com/16-mfungaji-aliyekula-au-kunywa-kwa-kusahau/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
