60 – Ahmad bin Naswr al-Khuzaa´iy (d. 231) – shahidi
220 – Imesihi ya kwamba Ibraahiym al-Harbiy ameeleza:
”Wakati Ahmad bin Naswr ameulizwa kuhusu ujuzi wa Allaah, akasema: ”Ujuzi wa Allaah uko nasi na Yeye yuko juu ya ´Arshi Yake.” Akaulizwa kuhusu Qur-aan ambapo akasema: ”Ni maneno ya Allaah.” Akaulizwa kama ni kiumbe ambapo akajibu: ”Hapana.”
61 – Mke wa Makkiy
221- Ahmad bin ´Aliy al-Abaar amesema: Muhammad bin ´Abdir-Rahmaan al-Balkhiy[1] ametuhadithia, Makkiy bin Ibraahiym amesema:
”Mke wa Jahm aliingia kwa mke wangu na akasema: ”Ee mama Ibraahiym, huyu ndiye mumeo anayezungumza kuhusu ´Arshi? Nani aliyeichonga?” Akajibu: ”Yule ambaye ameyachonga meno yako.”
Alikuwa na meno yaliyojitokeza kwa nje.
62 – Qutaybah bin Sa´iyd (150-240), shaykh wa Khuraasaan
222 – Abu Ahmad al-Haakim na mfasiri wa Qur-aan Abu Bakr an-Naqqaash, ambaye tamko ni lake, amesema: Abul-´Abbaas as-Sarraaj ametuhadithia: Nimemsikia Qutaybah bin Sa´iyd amesema:
”Hii ndio ´Aqiydah ya maimamu wa Uislamu na Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah: Tunamjua Mola wetu yuko juu ya mbingu ya saba juu ya ´Arshi Yake. Kama alivosema (´Azza wa Jall):
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[2]
Vivyo hivyo ndivo Muusa bin Harun alivyonukuu kutoka kwa Qutaybah, ambaye amesema:
” Tunamjua Mola wetu kuwa juu ya mbingu ya saba na juu ya ´Arshi Yake.”
Huyu hapa Qutaybah, ambaye anatambulika kwa uongozi na uaminifu wake, ambaye amenukuu maafikiano juu ya suala hili. Alikutana na Maalik, al-Layth, Hammaad bin Zayd na wakubwa wengine. Alikaa kwa muda mrefu na wanahifadhi wa Hadiyth walikuwa wakijazana kwenye mlango wake. Alimwambia mtu mmoja:
”Kaa nasi msimu huu wa baridi mpaka nikutolee kutoka kwa watu watano Hadiyth laki moja.”
Alifariki mwaka wa 240.
[1] Hivyo ndivyo ilivyoandikwa katika nakala zilizochapishwa na maandiko ya mkono. Naona kuwa ni kosa. Sahihi ni Muhammad bin ´Amr al-Balkhiy, kwani wamemtaja katika wapokezi wa Makkiy bin Ibraahiym. Naye ni Abu ´Abdillaah Muhammad bin ´Amr al-Balkhiy as-Swawwaaq ambaye ni mwenye kuaminika katika waalimu wa wa al-Bukhaariy, kama ilivyo kwa Makkiy bin Ibraahiym. al-Abaar ni mwaminifu pia, mwenye kuhifadhi na madhubuti, kama alivosema al-Khatwiyb (4/306).
[2] 20:5
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-´Uluww lil-´Aliy al-Ghaffaar, uk. 173-174
- Imechapishwa: 19/01/2026
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
60 – Ahmad bin Naswr al-Khuzaa´iy (d. 231) – shahidi
220 – Imesihi ya kwamba Ibraahiym al-Harbiy ameeleza:
”Wakati Ahmad bin Naswr ameulizwa kuhusu ujuzi wa Allaah, akasema: ”Ujuzi wa Allaah uko nasi na Yeye yuko juu ya ´Arshi Yake.” Akaulizwa kuhusu Qur-aan ambapo akasema: ”Ni maneno ya Allaah.” Akaulizwa kama ni kiumbe ambapo akajibu: ”Hapana.”
61 – Mke wa Makkiy
221- Ahmad bin ´Aliy al-Abaar amesema: Muhammad bin ´Abdir-Rahmaan al-Balkhiy[1] ametuhadithia, Makkiy bin Ibraahiym amesema:
”Mke wa Jahm aliingia kwa mke wangu na akasema: ”Ee mama Ibraahiym, huyu ndiye mumeo anayezungumza kuhusu ´Arshi? Nani aliyeichonga?” Akajibu: ”Yule ambaye ameyachonga meno yako.”
Alikuwa na meno yaliyojitokeza kwa nje.
62 – Qutaybah bin Sa´iyd (150-240), shaykh wa Khuraasaan
222 – Abu Ahmad al-Haakim na mfasiri wa Qur-aan Abu Bakr an-Naqqaash, ambaye tamko ni lake, amesema: Abul-´Abbaas as-Sarraaj ametuhadithia: Nimemsikia Qutaybah bin Sa´iyd amesema:
”Hii ndio ´Aqiydah ya maimamu wa Uislamu na Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah: Tunamjua Mola wetu yuko juu ya mbingu ya saba juu ya ´Arshi Yake. Kama alivosema (´Azza wa Jall):
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[2]
Vivyo hivyo ndivo Muusa bin Harun alivyonukuu kutoka kwa Qutaybah, ambaye amesema:
” Tunamjua Mola wetu kuwa juu ya mbingu ya saba na juu ya ´Arshi Yake.”
Huyu hapa Qutaybah, ambaye anatambulika kwa uongozi na uaminifu wake, ambaye amenukuu maafikiano juu ya suala hili. Alikutana na Maalik, al-Layth, Hammaad bin Zayd na wakubwa wengine. Alikaa kwa muda mrefu na wanahifadhi wa Hadiyth walikuwa wakijazana kwenye mlango wake. Alimwambia mtu mmoja:
”Kaa nasi msimu huu wa baridi mpaka nikutolee kutoka kwa watu watano Hadiyth laki moja.”
Alifariki mwaka wa 240.
[1] Hivyo ndivyo ilivyoandikwa katika nakala zilizochapishwa na maandiko ya mkono. Naona kuwa ni kosa. Sahihi ni Muhammad bin ´Amr al-Balkhiy, kwani wamemtaja katika wapokezi wa Makkiy bin Ibraahiym. Naye ni Abu ´Abdillaah Muhammad bin ´Amr al-Balkhiy as-Swawwaaq ambaye ni mwenye kuaminika katika waalimu wa wa al-Bukhaariy, kama ilivyo kwa Makkiy bin Ibraahiym. al-Abaar ni mwaminifu pia, mwenye kuhifadhi na madhubuti, kama alivosema al-Khatwiyb (4/306).
[2] 20:5
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-´Uluww lil-´Aliy al-Ghaffaar, uk. 173-174
Imechapishwa: 19/01/2026
Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/154-aqiydah-ya-maafikiano/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket