151. Juu ya ´Arshi Yake, hali ya kuwa ametengana na viumbe Wake?

54 – ´Abdul-Maalik bin al-Maajashuun (a.f.k. 214), mwanachuoni wa Madiynah

212 – Ibn Abiy Haatim amesema: Yahyaa bin Zakariyyaa bin ´Iysaa ametuhadithia: Haaruun bin Muusa al-Farawiy ametuhadithia:

”Sikuwahi kusikia mijadala kuhusu Qur-aan mpaka mwaka wa 209. Lililkuja kundi la watu kwa ´Abdul-Maalik bin al-Maajashuun na kuzungumza naye, ambapo akawakemea. Miongoni mwa mambo aliyowaambia: ”Je:

قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ

“Sema: ”Allaah ni Mmoja pekee.”[1]

ni kiumbe?” Kisha akasema: “Lau ningempata Bishr al-Mariysiy, basi ningemkata shingo yake.”[2]

´Abdul-Maalik alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi watukufu wa Maalik. Baba yake ´Abdul-´Aziyz bin al-Maajashuun alikuwa akitoa fatwa pamoja na Maalik katika serikali ya al-Mahdiy. ´Abdul-Malik alifariki mnamo 214.

213 – Abul-Hasan Muhammad bin al-´Attwaar amesema: Nimemsikia Muhammad bin Musw´ab al-´Aabid akisema:

“Yeyote anayesema eti Wewe huongei wala kuonekana Aakhirah, basi ni mwenye kukanusha uso Wako. Nashuhudia ya kwamba uko juu ya ´Arshi, juu ya mbingu saba, si kama wanavyosema maadui Zako mazanadiki.”[3]

Ameipokea ´Abdullaah bin Ahmad na Abu al-Hasan al-Daraaqutwniy.

214 – al-Marruudhiy amesema[4]: Nimemsikia Abu ´Abdillaah al-Khaffaaf akisema:

”Nimemsikia Ibn Mus’ab akisoma:

عَسَىٰ أَن يَبْعَثَكَ رَبُّكَ مَقَامًا مَّحْمُودًا

”Hapana shaka Mola wako atakuinua cheo kinachosifika.”[5]

“Ndiyo, atamkalisha pamoja Naye juu ya ´Arshi.”

Imaam Ahmad amemtaja Muhammad bin Mus´ab na akasema:

“Nimeandika kutoka kwake na ni mtu bora kiasi gani!”

Ama kuhusu suala la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuketi juu ya ´Arshi hakuna maandiko yaliyothibiti katika hilo. Bali ipo Hadiyth nyonge juu ya suala hilo[6].

[1] 112:1

[2] Cheni yake ya wapokezi ni Swahiyh. Ibn Abiy Haatim ameandika wasifu wa huyu Ibn ´Iysaa na akasema:

”Nimeandika kutoka kwake pamoja na baba yangu. Naye ni mkweli na mwenye kuaminika.”  (al-Jarh wat-Ta´diyl (4/2/146))

Wasifu wa al-Farawiy umeandikwa katika “at-Tahdhiyb”.

[3] as-Sunnah, uk. 34. al-Khatwiyb ameipokea kupitia kwa ad-Daaraqutwniy kisha akasimulia kwamba Ibn Sa´d amesema:

“Abu Ja´far Muhammad bin Mus´ab alikuwa ni msomaji wa Qur-aan, alizisikia Hadiyth na akaketi na watu.  Alikuwa –  Allaah akitaka – mwenye kuaminika. Alifariki mnamo 228 huko Baghdaad.” (Taariykh Baghdaad (3/280))

Huyu sio Muhammad bin Mus´ab al-Qarqasaaniy.

al-Khatwiyb ameandika wasifu wa Muhammad bin al-´Attwaar na akapokea  ya kwamba ´Abdullaah bin Ahmad amesema kwamba alikuwa “mwenye kuaminika” (Taariykh Baghdaad (3/203-204)).

Cheni yake ya wapokezi ni Swahiyh. Mtunzi pia ameisahihisha katika ufupisho wake.

[4] Katika toleo fupi kurejelewe ”Fadhwiylat-un-Nabiy”.

[5]17:79

[6] Hata hivyo ni kwamba Hadiyth Swahiyh inasema kwamba cheo chenye kusifiwa ni ule uombezi mkubwa wa Mtume wetu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), ambao ni maalum kwake.

  • Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-´Uluww lil-´Aliy al-Ghaffaar, uk. 169-171
  • Imechapishwa: 19/01/2026
  • Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy