Nia katika ´ibaadah zote mahali pake ni moyoni. Kwa msemo mwingine haijuzu kuitamka kwa sauti, kwa sababu hilo halikupokewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wala kutoka kwa Maswahabah wake kwamba walikuwa wakisema:
”Nimekusudia kufunga.”
”Nimekusudia kuswali.”
Kwa hiyo kuitamka nia kwa sauti ni Bid´ah iliyozuliwa. Inatosha katika nia kula na kunywa kwa kusudia kufunga. Shaykh Taqiyy-ud-Diyn Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema:
“Yeye anapokula chakula cha usiku anakula chakula cha mtu anayekusudia kufunga, kwa sababu hiyo hutofautishwa kati ya chakula cha usiku wa ´iyd na chakula cha nyusiku za Ramadhaan.”
Amesema pia:
“Kila anayejua kuwa kesho ni Ramadhaan na anataka kuifunga, basi ameshaweka nia, jambo ambalo ndio kitendo cha waislamu wengi.”
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ithaaf Ahl-il-Iymaan bi Duruus Shahri Ramadhwaan, uk. 22
- Imechapishwa: 05/02/2026
Nia katika ´ibaadah zote mahali pake ni moyoni. Kwa msemo mwingine haijuzu kuitamka kwa sauti, kwa sababu hilo halikupokewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wala kutoka kwa Maswahabah wake kwamba walikuwa wakisema:
”Nimekusudia kufunga.”
”Nimekusudia kuswali.”
Kwa hiyo kuitamka nia kwa sauti ni Bid´ah iliyozuliwa. Inatosha katika nia kula na kunywa kwa kusudia kufunga. Shaykh Taqiyy-ud-Diyn Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema:
“Yeye anapokula chakula cha usiku anakula chakula cha mtu anayekusudia kufunga, kwa sababu hiyo hutofautishwa kati ya chakula cha usiku wa ´iyd na chakula cha nyusiku za Ramadhaan.”
Amesema pia:
“Kila anayejua kuwa kesho ni Ramadhaan na anataka kuifunga, basi ameshaweka nia, jambo ambalo ndio kitendo cha waislamu wengi.”
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ithaaf Ahl-il-Iymaan bi Duruus Shahri Ramadhwaan, uk. 22
Imechapishwa: 05/02/2026
https://firqatunnajia.com/15-kutamka-nia-kwa-sauti-ni-bidah/
Mshirikishe mwenzako:
- Share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Print (Opens in new window) Print
- Email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Share on X (Opens in new window) X
- Share on Pocket (Opens in new window) Pocket