54 – ´Abdullaah bin ´Amr bin al-´Aasw (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
اللَّهُمَّ مُصَرِّفَ القُلُوبِ صَرِّفْ قُلُوبَنَا علَى طَاعَتِكَ
“Ee Allaah! Mwenye kuzipindua nyoyo, Upindue moyo wangu katika utiifu Wako.”[1]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Hapa kuna fadhilah za du´aa hii:
اللَّهُمَّ مُصَرِّفَ القُلُوبِ صَرِّفْ قُلُوبَنَا علَى طَاعَتِكَ
“Ee Allaah! Mwenye kuzipindua nyoyo, Upindue moyo wangu katika utiifu Wako.”
Hadiyth nyingine Umm Salamah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
“Du´aa yake alikuwa akiomba kwa wingi ilikuwa:
يَا مُقَلِّبَ القُلُوبِ ثَبِّتْ قَلْبِي عَلَى دِينِكَ
“Ee Mwenye kuzipindua nyoyo, Uthibitishe moyo wangu katika dini yako.”
Nikasema: “Ee Mtume wa Allaah! Ni kwa wingi uliyoje unaomba:
يَا مُقَلِّبَ القُلُوبِ ثَبِّتْ قَلْبِي عَلَى دِينِكَ
“Ee Mwenye kuzipindua nyoyo, Uthibitishe moyo wangu katika dini yako?”
Akasema: “Ee Umm Salamah! Hakuna mwanadamu yeyote isipokuwa moyo wake uko kati ya vidole viwili katika vidole vya Allaah; Anaoutaka anaunyoosha na Anaoutaka anaupindisha.”[2]
Yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anaomba hivi licha ya kwamba ndiye bwana wa viumbe. Kwa hiyo inampasa muislamu aomba kwa wingi du´aa hii.
[1] Muslim (2654).
[2] at-Tirmidhiy (3522).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 61
- Imechapishwa: 20/10/2025
54 – ´Abdullaah bin ´Amr bin al-´Aasw (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
اللَّهُمَّ مُصَرِّفَ القُلُوبِ صَرِّفْ قُلُوبَنَا علَى طَاعَتِكَ
“Ee Allaah! Mwenye kuzipindua nyoyo, Upindue moyo wangu katika utiifu Wako.”[1]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Hapa kuna fadhilah za du´aa hii:
اللَّهُمَّ مُصَرِّفَ القُلُوبِ صَرِّفْ قُلُوبَنَا علَى طَاعَتِكَ
“Ee Allaah! Mwenye kuzipindua nyoyo, Upindue moyo wangu katika utiifu Wako.”
Hadiyth nyingine Umm Salamah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
“Du´aa yake alikuwa akiomba kwa wingi ilikuwa:
يَا مُقَلِّبَ القُلُوبِ ثَبِّتْ قَلْبِي عَلَى دِينِكَ
“Ee Mwenye kuzipindua nyoyo, Uthibitishe moyo wangu katika dini yako.”
Nikasema: “Ee Mtume wa Allaah! Ni kwa wingi uliyoje unaomba:
يَا مُقَلِّبَ القُلُوبِ ثَبِّتْ قَلْبِي عَلَى دِينِكَ
“Ee Mwenye kuzipindua nyoyo, Uthibitishe moyo wangu katika dini yako?”
Akasema: “Ee Umm Salamah! Hakuna mwanadamu yeyote isipokuwa moyo wake uko kati ya vidole viwili katika vidole vya Allaah; Anaoutaka anaunyoosha na Anaoutaka anaupindisha.”[2]
Yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anaomba hivi licha ya kwamba ndiye bwana wa viumbe. Kwa hiyo inampasa muislamu aomba kwa wingi du´aa hii.
[1] Muslim (2654).
[2] at-Tirmidhiy (3522).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 61
Imechapishwa: 20/10/2025
https://firqatunnajia.com/15-duaa-ya-kumuomba-allaah-authibitishe-moyo-wako-katika-dini-yake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
