72 – ´Ubayd al-Muktib amesimulia kutoka kwa Mujaahid ambaye ameeleza kuwa ´Abdullaah bin ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
”Allaah ameumba vitu vinne kwa mkono Wake: Aadam, kalamu, ´Arshi na Pepo ya Edeni. Akaviambia viumbe vyengine vyote: ”Kuwa!” na vikawa.”[1]
73 – Imesihi kwamba ´Abdullaah bin ´Amr bin al-´Aasw amesema:
”Malaika walisema: ”Ee Mola wetu! Miongoni mwetu wako waliokurubishwa, wengine wenye kubeba ´Arshi na wengine ni waandishi watukufu. Umewaumba wanaadamu na ukawapa dunia; nasi tupe Aakhirah.” Akasema: ”Sintofanya kizazi cha ambaye nimemuumba kwa mkono Wangu kuwa kama ambaye nimemuumba kwa kusema ”Kuwa!” na akawa.”
75 – Jaabir ameipokea hiyohiyo kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
76 – Imethibiti kwamba Abu Hurayrah amesema:
”Allaah alisema kumwambia Aadam na huku mikono Yake miwili ikiwa wazi: ”Chagua unaotaka.” Akasema: ”Nachagua mkono wa kuume wa Mola wangu.”[2]
77 – Imesihi kwamba al-Mughiyrah bin Shu´bah amesema:
”Muusa alimuuliza Mola wake: ”Ee Mola! Nieleze mtu wa Peponi ambaye yuko na nafasi ya juu kabisa?” Akasema: ”Wale ambao heshima yao Nimeipanda kwa mkono Wangu na nikaipiga muhuri; hakuna jicho limekwishaiona, hakuna sikio limekwishaisikia na wala haijapita kwenye moyo wa yeyote.”[3]
Ameipokea Muslim.
78 – Imesihi kutoka kwa Ismaa´iyl bin Abiy Khaalid, kutoka kwa al-Hakiym bin Jaabir ambaye amesema:
”Nimekuelezeni kuwa Mola wenu hakuna kitu alichokigusa kwa mkono Wake isipokuwa vitu vitatu: Alipanda Pepo kwa mkono Wake, akamuumba Aadam kwa mkono Wake na akaandika Tawraat kwa mkono Wake.”
78 – Mfano wa hayo yamesihi kutoka kwa Mughiyth bin Sumayy.
79 – Imesihi kutoka kwa Naafiy´ bin ´Umar al-Jamhiy ambaye amesema:
”Nilimuuliza Ibn Abiy Mulaykah kama Allaah ana mkono mmoja au miwili. Akajibu: ”Miwili.”[4]
Endapo nitazitaja Hadiyth zote zinazotaja mikono miwili ya Allaah, basi kitakuwa kirefu.
[1] al-Bayhaqiy katika ”al-Asmaa’ was-Swifaat” (693), al-Haakim (2/319), ash-Shariy´ah, uk. 313, na wengineo.
[2] al-Haakim aliyesema:
”Hadiyth ni Swahiyh kwa mujibu wa sharti za Muslim.” (al-Mustadrak (1/64))
[3] Muslim (312), at-Tirmidhiy (3198) na al-Bayhaqiy (690).
[4] ar-Radd ´alaa Bishr al-Mariysiy, uk. 38
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 78-81
- Imechapishwa: 04/06/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)