44 – al-Khuraybiy (126-213), mmoja katika maimamu wa masimulizi
191 – ´Aliy bin Abiyr-Rabiy´ al-Bazzaar amesema:
”Nilimwendea Bishr bin al-Haarith na kusema: ”Ee Abu Naswr! Umesikia chochote kuhusu Qur-aan?” Akasema: ”Nilimuuliza ´Abdullaah bin Daawuud al-Khuraybiy kuhusu hilo, kisha akanisomea mwisho wa ”al-Hashr”:
هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ
”Yeye ni Allaah, ambaye hakuna mungu wa haki isipokuwa Yeye.”[1]
Kisha akasema: ”Je, hili ni kiumbe?” Ulinzi unaombwa kwa Allaah!”[2]
192 – ´Abdullaah bin Muhammad bin Asmaa’ amesimulia kwamba al-Khuraybiy amesema:
”Wakati nilipokuwa natembea Abadan na nikawa naihadithia nafsi yangu juu ya uumbwaji wa Qur-aan, mtu mmoja akanishika kwa nyuma yangu, akanitikisa na kusema: ”Ee mwana wa Daawuud, kuwa imara! Hakika maneno ya Allaah si kiumbe.” Nikageuka na simuona yeyote.”[3]
[1] 59:23
[2] Cheni yake ya wapokezi ni dhaifu.
[3] Ibn Asmaa´ ni madhubuti, mtukufu na ni miongoni mwa wasimulizi wa al-Bukhaariy na Muslim. Ikiwa cheni ya wapokezi imesihi hadi kwake, basi masimulizi nayo ni Swahiyh. Hata hivyo sijapata chochote juu yake hadi sasa.
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-´Uluww lil-´Aliy al-Ghaffaar, uk. 160-161
- Imechapishwa: 12/01/2025
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
44 – al-Khuraybiy (126-213), mmoja katika maimamu wa masimulizi
191 – ´Aliy bin Abiyr-Rabiy´ al-Bazzaar amesema:
”Nilimwendea Bishr bin al-Haarith na kusema: ”Ee Abu Naswr! Umesikia chochote kuhusu Qur-aan?” Akasema: ”Nilimuuliza ´Abdullaah bin Daawuud al-Khuraybiy kuhusu hilo, kisha akanisomea mwisho wa ”al-Hashr”:
هُوَ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ
”Yeye ni Allaah, ambaye hakuna mungu wa haki isipokuwa Yeye.”[1]
Kisha akasema: ”Je, hili ni kiumbe?” Ulinzi unaombwa kwa Allaah!”[2]
192 – ´Abdullaah bin Muhammad bin Asmaa’ amesimulia kwamba al-Khuraybiy amesema:
”Wakati nilipokuwa natembea Abadan na nikawa naihadithia nafsi yangu juu ya uumbwaji wa Qur-aan, mtu mmoja akanishika kwa nyuma yangu, akanitikisa na kusema: ”Ee mwana wa Daawuud, kuwa imara! Hakika maneno ya Allaah si kiumbe.” Nikageuka na simuona yeyote.”[3]
[1] 59:23
[2] Cheni yake ya wapokezi ni dhaifu.
[3] Ibn Asmaa´ ni madhubuti, mtukufu na ni miongoni mwa wasimulizi wa al-Bukhaariy na Muslim. Ikiwa cheni ya wapokezi imesihi hadi kwake, basi masimulizi nayo ni Swahiyh. Hata hivyo sijapata chochote juu yake hadi sasa.
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-´Uluww lil-´Aliy al-Ghaffaar, uk. 160-161
Imechapishwa: 12/01/2025
Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/142-kuwa-imara/