Qadar ina ngazi nne ambazo ni lazima kuziamini zote:
Ngazi ya kwanza: Kuamini kwamba Allaah alikijua kila kitu kwa ujuzi Wake wa milele ambayo anasifika kwayo milele na siku zote. Ngazi hii ndio waliyoipinga Qadariyyah waliochupa mpaka.
Ngazi ya pili: Kuamini kwamba Allaah ameandika katika Ubao uliohifadhiwa kila kitu. Hayo ni kutokana na Hadiyth:
“Kitu cha kwanza alichoumba Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) ni kalamu. Kisha akaiambia: “Andika!” Ikasema: “Niandike nini?” Akasema: “Andika yatayokuwa na yatayokuweko mpaka Qiyaamah kisimame.”[1]
Allaah (Jalla wa ´Alaa) anasema:
مَا أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي أَنفُسِكُمْ إِلَّا فِي كِتَابٍ
“Hausibu msiba wowote katika ardhi au katika nafsi zenu isipokuwa upo katika Kitabu… “
Kitabu ni Ubao uliohifadhiwa.
مِّن قَبْلِ أَن نَّبْرَأَهَا
“… kabla hatujautokezesha.”
Bi maana kabla ya kuumba.
إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرٌ
“Hakika hayo kwa Allaah ni mepesi.”[2]
Uandikaji:
“Kabla ya kuumba mbingu na ardhi kwa miaka 50.000 na ´Arhi Yake ilikuwa juu ya maji.”
Uandikaji ulitangulia kitambo kabla ya kuumbwa mbingu na ardhi.
Ngazi ya tatu: Matakwa na utashi: Kila kitu kinachotokea ni kwa kutaka kwa Allaah. Hapa kuna Radd kwa Qadariyyah. Hakukuwi katika ufalme Wake (Subhaanahu wa Ta´ala) yale asiyoyataka Allaah:
وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ مَا اقْتَتَلُوا وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَفْعَلُ مَا يُرِيدُ
“Lau angelitaka Allaah wasingelipigana lakini Allaah anafanya atakavyo.”[3]
إِنَّ اللَّـهَ يَفْعَلُ مَا يَشَاءُ
“Hakika Allaah anafanya atakavyo.”[4]
Kila kitu kinachotokea Allaah amekitaka baada ya kukijua na kukiandika katika Ubao uliohifadhiwa.
Ngazi ya nne: Uumbaji: Amekijua, akakiandika na akakikuumba (Subhaanahu wa Ta´ala).
Ni lazima uamini ngazi zote hizi. Vinginevyo utakuwa si mwenye kuamini mipango na makadirio ya Allaah.
[1] Abu Daawuud (4700), at-Tirmidhiy (2155, 3319), Ahmad katika ”al-Musnad” (05/317, nambari. 22705, 22707) kupitia kwa ´Ubaadah bin as-Swaamitw (Radhiya Allaahu ´anh).
[2] 57:22
[3] 02:253
[4] 22:18
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Aqiydat-il-Imaam Mujaddid Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab, uk. 32-33
- Imechapishwa: 08/03/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)