7 – Miongoni mwa shubuha zao wanasema kusherehekea maulidi na kusoma historia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika mnasaba huu kuna mahamasisho ya kumuiga na kumtii. Tunawajibu kwa kuwaambia kuwa kusoma historia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kitu kinachotakikana kwa kila muislamu katika maisha yake yote. Lakini kufanya hivo kwa kuhusiaha siku maalum – pasi na kuwepo dalili ya umaalum huo – ni jambo la Bid´ah:

“Kila Bid´ah ni upotevu.”

Bid´ah haizai isipokuwa shari tupu na kumuweka mtu mbali na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Huquwq-un-Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) bayn al-Ijlaal wal-Ikhlaal, uk. 156
  • Imechapishwa: 06/09/2025