Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
9- Mawazo hayawezi kumfikia, fahamu haziwezi kumzunguka Yeye.
MAELEZO
Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) hawezi kuzungukwa. Yeye ni mkubwa kabisa kuliko kila kitu:
يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ وَلَا يُحِيطُونَ بِهِ عِلْمًا
“Anajua yale yaliyoko mbele yao na yale yaliyoko nyuma yao na wala hawawezi kumzunguka Yeye wote kiujuzi.”[1]
Upande mmoja kuna elimu kumuhusu Allaah. Upande mwingine hawezi kuzungukwa. Yeye ni mkubwa kuliko kila kitu. Mawazo hayawezi kumfikiria. Wala haijuzu kusema kitu kumuhusu isipokuwa yale yaliyosemwa na Allaah (Subhaanah) au yakasemwa na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] 20:110
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 37
- Imechapishwa: 11/09/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)