Kuhusu tafsiri ya Qur-aan watu wenye ujuzi ni wa Makkah. Kwa sababu walikuwa ni maswahiba wa Ibn ‘Abbaas, kama vile Mujaahid, ‘Atwaa bin Abiy Rabbaah, ‘Ikrimah – aliyekuwa mjakazi wa Ibn ‘Abbaas – na wengineo kama vile Twaawuus, Abu ash-Sha’thaa’, Sa´iyd bin Jubayr na mfano wao. Vivyo hivyo watu wa Kuufah katika maswahiba wa Ibn Mas’uud, jambo ambalo liliwapambanua kutokana na wengine. Wanazuoni wa Madiynah katika tafsiri ya Qur-aan ikiwa ni pamoja na Zayd bin Aslam, ambaye Maalik na mwanaye ´Abdur-Rahmaan walisoma kwake tafsiri ya Qur-aan, kisha ‘Abdullaah bin Zayd, kisha baada ya hapo ´Abdullaah bin Wahb akasoma tafsiri ya Qur-aan kusoma ´Abdur-Rahmaan.
- Muhusika: Shaykh-ul-Islaam Ahmad bin Taymiyyah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Muqaddimah fiy Usuwl-it-Tafsiyr, uk. 54
- Imechapishwa: 01/04/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)