al-Qaadhwiy Abu Yuusuf (afk. 182 – Rahimahu Allaah).
157 – Imethibiti kwamba Abu Yuusuf (Rahimahu Allaah) amesema:
”Yeyote mwenye kutafuta dini katika falsafa atakuwa zandiki. Yeyote mwenye kutafuta mali kwa kemia atafilisika. Yeyote mwenye kufuatiliafuatilia maongezi ya kigeni ataongopea.”[1]
158 – Bashshaar bin Muusa al-Khaffaaf amesema:
”Bishr al-Waliyd al-Kindiy alikuja kwa Abu Yuusuf na kumwambia: ”Unanikataza falsafa wakati ambapo Bishr al-Mariysiy na ´Aliy al-Ahwal wote wawili wanazungumza?” Akasema: ”Wanasema nini?” Wakasema: ”Allaah yuko kila mahali.” Abu Yuusuf akasema: ”Basi nitawashughulikia.” Walipoletwa kwake mahali alipo, Bishr akasimama na ´Aliy al-Ahwal akasogezwa mbele na mzee mmoja. Abu Yuusuf akamtazama yule mzee na kusema: ”Kama usingelikuwa mtu unayetakiwa kufanyiwa adabu basi ningekuumiza.” Akaamrisha afungwe, akampiga al-Ahwal na akaamrisha azungushwe kati ya watu.”[2]
159 – ´Aliy bin al-Hasan al-Kuraa´iy ameeleza kuwa Abu Yuusuf amesema:
”Nimejadiliana na Abu Haniyfah miezi sita na tukaafikiana juu ya kwamba yeyote mwenye kusema kuwa Qur-aan ni kiumbe ni kafiri.”[3]
160 – Bashshaar al-Khaffaaf ameeleza kuwa amemsikia Abu Yuusuf akisema:
”Yeyote mwenye kusema kuwa Qur-aan ni kiumbe atengwe.”[4]
[1] Ameipokea al-Harawiy katika “Dhamm-ul-Kalaam” (6/104/1) kupitia njia mbili kutoka kwa Abu Yuusuf. Ibn Taymiyyah amethibitisha katika “al-Jawaab al-Faaswil” kuwa ni masimulizi yenye kutoka kwake. al-Harawiy (5/94/2) amepokea mfano wake kutoka kwa Maalik.
[2] Mtunzi ameipokea kupitia kwa Haafidhw Ibn Abiy Haatim: al-Hasan bin ´Aliy bin Mihraan: Bashshaar bin Muusa al-Khaffaaf ametukhabarisha. Bashshaar ni dhaifu na ni mwenye kukosea sana.
[3] Mtunzi ameisimulia kupitia kwa Ibn Abiy Haatim: Ahmad bin Muhammad bin Muslim ametuhadithia: ´Aliy bin al-Hasan al-Kuraa´iy ametuhadithia. Cheni yake ya wapokezi ni nzuri.
[4] Bashshaar ni mnyonge kama ilivyokwishatangulia.
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-´Uluww lil-´Aliy al-Ghaffaar, uk. 151-152
- Imechapishwa: 21/07/2024
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
al-Qaadhwiy Abu Yuusuf (afk. 182 – Rahimahu Allaah).
157 – Imethibiti kwamba Abu Yuusuf (Rahimahu Allaah) amesema:
”Yeyote mwenye kutafuta dini katika falsafa atakuwa zandiki. Yeyote mwenye kutafuta mali kwa kemia atafilisika. Yeyote mwenye kufuatiliafuatilia maongezi ya kigeni ataongopea.”[1]
158 – Bashshaar bin Muusa al-Khaffaaf amesema:
”Bishr al-Waliyd al-Kindiy alikuja kwa Abu Yuusuf na kumwambia: ”Unanikataza falsafa wakati ambapo Bishr al-Mariysiy na ´Aliy al-Ahwal wote wawili wanazungumza?” Akasema: ”Wanasema nini?” Wakasema: ”Allaah yuko kila mahali.” Abu Yuusuf akasema: ”Basi nitawashughulikia.” Walipoletwa kwake mahali alipo, Bishr akasimama na ´Aliy al-Ahwal akasogezwa mbele na mzee mmoja. Abu Yuusuf akamtazama yule mzee na kusema: ”Kama usingelikuwa mtu unayetakiwa kufanyiwa adabu basi ningekuumiza.” Akaamrisha afungwe, akampiga al-Ahwal na akaamrisha azungushwe kati ya watu.”[2]
159 – ´Aliy bin al-Hasan al-Kuraa´iy ameeleza kuwa Abu Yuusuf amesema:
”Nimejadiliana na Abu Haniyfah miezi sita na tukaafikiana juu ya kwamba yeyote mwenye kusema kuwa Qur-aan ni kiumbe ni kafiri.”[3]
160 – Bashshaar al-Khaffaaf ameeleza kuwa amemsikia Abu Yuusuf akisema:
”Yeyote mwenye kusema kuwa Qur-aan ni kiumbe atengwe.”[4]
[1] Ameipokea al-Harawiy katika “Dhamm-ul-Kalaam” (6/104/1) kupitia njia mbili kutoka kwa Abu Yuusuf. Ibn Taymiyyah amethibitisha katika “al-Jawaab al-Faaswil” kuwa ni masimulizi yenye kutoka kwake. al-Harawiy (5/94/2) amepokea mfano wake kutoka kwa Maalik.
[2] Mtunzi ameipokea kupitia kwa Haafidhw Ibn Abiy Haatim: al-Hasan bin ´Aliy bin Mihraan: Bashshaar bin Muusa al-Khaffaaf ametukhabarisha. Bashshaar ni dhaifu na ni mwenye kukosea sana.
[3] Mtunzi ameisimulia kupitia kwa Ibn Abiy Haatim: Ahmad bin Muhammad bin Muslim ametuhadithia: ´Aliy bin al-Hasan al-Kuraa´iy ametuhadithia. Cheni yake ya wapokezi ni nzuri.
[4] Bashshaar ni mnyonge kama ilivyokwishatangulia.
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-´Uluww lil-´Aliy al-Ghaffaar, uk. 151-152
Imechapishwa: 21/07/2024
Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/126-mjadala-miezi-sita-na-abu-haniyfah/