Hajj yenye kukubaliwa ina sifa zifuatazo:
1 – Kuwa matumizi yote ni kutoka katika mali halali. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika Allaah ni Mzuri na wala hakubali isipokuwa kilicho kizuri…”[1]
Ameipokea Muslim.
2 – Kumtakasia matendo Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) na kufuata Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
3 – Kujiepusha kabisa na maasi na madhambi, pamoja na Bid´ah na mambo yanayoenda kinyume na Shari´ah.
4 – Tabia njema, unyenyekevu, huruma kwa wengine na kutojikweza katika mavazi au kipando, katika kutangamana na watu wengine, kama alivyokuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Hajj yake. Ibn ´Abdil-Barr (Rahimahu Allaah) amesema:
“Hajj yenye kukubaliwa ni ile isiyokuwa kujionyesha, kutaka kusikika, matusi na jimaa wala ufuska na ifanywe kwa mali halali…”[2]
[1] Ameipokea Muslim (1015).
[2] at-Tamhiyd (22/39).
- Muhusika: Shaykh ´Abdullaah bin Swaalih al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahaadiyth ´Ashrah Dhil-Hijjah wa Ayaam-it-Tashriyq, uk. 18
- Imechapishwa: 11/05/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket