48 – Muhammad bin Abiy ´Aliy al-Aswbahaaniy alitusomea mashairi:
Ee mwanaume! Ifanyie kazi elimu yako utashinda
Elimu hainufaishi kitu bila ya matendo mema
Elimu ni pambo na kumcha Allaah ndio pambo lake
Wale wanaomcha Allaah wanajishughulisha na elimu
Ee mwenye elimu! Hoja ya Allaah ni yenye kushinda!
Si vitimbi wala hila zinanufaisha dhidi yake
Jifunze elimu na uifanyie kazi vile unavyoweza
Usiache upuuzi na mabishano yakakushughulisha kuitafuta kwake
Wafunze watu na ukusudie kuwanufaisha
Na tahadhari kwelikweli usichoke
Muwaidhi ndugu yako kwa upole kutokana na kosa lake,
kwa sababu yule aliyefungana na elimu hutumbukia kwenye kosa
Unapokuwa kati ya watu walionyimwa
basi waamrishe mema ikiwa hawajui
Wasipokutii warejelee bila kukereka
Subiri na uvute subira na usihuzunike kwa wanayoyafanya
Kila mwana-kondoo amesimamishwa kwa miguu yake na ikiwa
watashikilia dhuluma na kudhulumu basi jiweke kivyako
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Iqtidhwaa’-ul-´Ilm al-´Amal, uk. 38-39
- Imechapishwa: 12/05/2024
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket