… na akavifungua vifua vyao kwa ajili ya ukumbusho – Pindi Allaah anapotaka kumwongoza mtu basi hukifungua kifua chake ambapo akakubali wito kwa Allaah (´Azza wa Jall). Amesema (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
فَمَن يُرِدِ اللَّـهُ أَن يَهْدِيَهُ يَشْرَحْ صَدْرَهُ لِلْإِسْلَامِ
“Basi yule ambaye Allaah anataka kumwongoza, humfungulia kifua chake kwa Uislamu… “
Anakuwa ni mwenye kukubali na mwenye shauku na hivyo Allaah anakifungua kifua chake juu ya Uislamu. Huu ni utashi wa kilimwengu:
وَمَن يُرِدْ أَن يُضِلَّهُ يَجْعَلْ صَدْرَهُ ضَيِّقًا حَرَجًا
“… na yule ambaye anataka kumpotoa, basi hufanya kifua chake kuwa na dhiki chenye uzito.”[1]
Huu pia ni utashi wa kilimwengu. Anakuwa si mwenye kukubali kitu. Hapendi kheri. Anakimbia mbali na kheri na watu wa kheri:
كَأَنَّمَا يَصَّعَّدُ فِي السَّمَاءِ
“… kama kwamba anapanda kwa tabu mbinguni.”[2]
Kifua chake kinakuwa chenye dhiki. Wanahisi dhiki kutokamana na haki, ulinganizi kwa Allaah, usomwaji wa Qur-aan, mawaidha na ukumbusho. Kwa sababu Allaah amefanya vifua vyao kuwa vyenye dhiki kwa ajili ya kuwaadhibu kutokana na kupuuzia kwao. Hivyo Allaah anawanyima uongofu.
[1] 06:125
[2] 6:125
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bayaan-ul-Ma´aaniy fiy Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy, uk. 16
- Imechapishwa: 05/07/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)