1- Inafaa kwa msafiri kula katika mwezi wa Ramadhaan katika kile kipindi cha safari yake kisha alipe baadaye alipe zile siku alizokula. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ
“Atakayekuwa mgonjwa au safarini, basi atimize idadi katika masiku mengine.”[1]
2- Msafiri aliyefunga katika mwezi wa Ramadhaan amekhiyarishwa kati ya kufunga na kula. Hata hivyo akila atatakiwa kulipa. Hayo ni kutokana na yale yaliyothibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim kupitia kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ambaye amesimulia kuwa Hamzah bin ´Imraan al-Aslamiy alisema kumwambia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Je, nifunge nikiwa safarini?” – mtu huyu alikuwa ni mwenye kufunga sana – akamjibu: “Ukitaka funga na ukitaka kula.”[2]
[1] 02:185
[2] al-Bukhaariy (1943) na Muslim (1121).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mukhtaswaru fiy Ahkaam-is-Swiyaam, uk. 17
- Imechapishwa: 18/04/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket