Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“´Umrah moja hadi ´Umrah nyingine ni kafara kwa madhambi yaliyoko baina yake na Hajj yenye kukubaliwa haina malipo mengine isipokuwa Pepo.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Hii Hadiyth ni dalili ya fadhilah ya Hajj yenye kukubaliwa na ujira wake mkubwa mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala), kwani mwenye kuitekeleza kwa hali hiyo atakuwa miongoni mwa waliopata radhi za Allaah na Pepo Yake.
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) pia amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliulizwa:
“Ni kitendo gani kilicho bora zaidi?” Akasema: “Kumwamini Allaah na Mtume Wake.” Akaulizwa: “Kisha kipi?” Akasema: “Kupambana Jihaad katika njia ya Allaah.” Akaulizwa: “Kisha kipi?” Akasema: “Hajj yenye kukubaliwa.”[2]
Kuna maafikiano juu yake.
[1] al-Bukhaariy (1683) na Muslim (1349).
[2] al-Bukhaariy (16, 1447) na Muslim (83).
- Muhusika: Shaykh ´Abdullaah bin Swaalih al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahaadiyth ´Ashrah Dhil-Hijjah wa Ayaam-it-Tashriyq, uk. 18
- Imechapishwa: 10/05/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket