al-Bayhaqiy (2/431) amesema: Abul-Husayn bin Bishraan al-´Adl ametufahamisha Baghdaad: Ismaa´iyl bin Muhammad as-Swaffaar ametuhadithia: Sa´daan bin Naswr ametuhadithia: Abu Badr ametuhadithia, kutoka kwa Ziyaad bin Khaythamah, kutoka kwa ´Abdullaah bin ´Iysaa, kutoka kwa ´Abdullaah bin ´Atwaa’, kutoka kwa ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa), ambaye amesema:
”Nilimuona Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiswali akiwa peku na amevaa viatu, akinywa akiwa amekaa na amesimama, akimaliza kuswali anageuka kulia au kushoto, pasi na kujali anafanya hivo upande gani.”
al-Haythamiy amesema kuhusu Hadiyth:
”Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Awsatw”. Wanaume wake ni wenye kuaminika.”[1]
Tofauti pekee iliopo ni kwamba imekuja katika kitabu chake ”na anaondoka zake” badala ya ”akimaliza kuswali anageuka kulia… ”
[1] Majma´-uz-Zawaa’id (2/55).
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: as-Swalaah fiyn-Ni´aal, uk. 13
- Imechapishwa: 02/06/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket