Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
86 – Endapo viumbe wote watakusanyika kuzuia kitu ambacho Allaah (Ta´ala) amekwishahukumu kutokea kwake, basi hawatoweza. Na endapo wote watakusanyika kukileta kitu ambacho Allaah (Ta´ala) hajahukumu kutokea kwake, basi hawatoweza.
MAELEZO
Hakuna yeyote anayeweza kubadilisha yale aliyoyaandika Allaah katika Ubao uliohifadhiwa. Lau viumbe wote watakusanyika kubadilisha kitu ambacho Allaah amekwishakiandika, basi hawatofanikia, na lau wote watakusanyika kukileta kitu ambacho Allaah hakukiandikia kwenye Ubao uliohifadhiwa, basi hawatoweza. Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Jua ya kwamba ikiwa taifa zima litaungana kukunufaisha wewe kwa kitu, basi hutonufaika isipokuwa kwa kitu alichokwishakuandikia Allaah. Kadhalika wakikusanyika kukudhuru kwa chochote, basi howatokudhu isipokuwa tu kwa kitu alichokwishakuandikia. Kwani kalamu zimeshanyanyuliwa na sahifa zimeshakauka.”[1]
Hakuna mabadiliko wala mageuzi wa yale aliyoyaandika Allaah (Jalla wa ´Alaa) katika Ubao uliohifadhiwa.
[1] Ahmad (1/307) na at-Tirmidhiy (2516) ambaye amesema:
”Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 117
- Imechapishwa: 05/11/2024
Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
86 – Endapo viumbe wote watakusanyika kuzuia kitu ambacho Allaah (Ta´ala) amekwishahukumu kutokea kwake, basi hawatoweza. Na endapo wote watakusanyika kukileta kitu ambacho Allaah (Ta´ala) hajahukumu kutokea kwake, basi hawatoweza.
MAELEZO
Hakuna yeyote anayeweza kubadilisha yale aliyoyaandika Allaah katika Ubao uliohifadhiwa. Lau viumbe wote watakusanyika kubadilisha kitu ambacho Allaah amekwishakiandika, basi hawatofanikia, na lau wote watakusanyika kukileta kitu ambacho Allaah hakukiandikia kwenye Ubao uliohifadhiwa, basi hawatoweza. Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Jua ya kwamba ikiwa taifa zima litaungana kukunufaisha wewe kwa kitu, basi hutonufaika isipokuwa kwa kitu alichokwishakuandikia Allaah. Kadhalika wakikusanyika kukudhuru kwa chochote, basi howatokudhu isipokuwa tu kwa kitu alichokwishakuandikia. Kwani kalamu zimeshanyanyuliwa na sahifa zimeshakauka.”[1]
Hakuna mabadiliko wala mageuzi wa yale aliyoyaandika Allaah (Jalla wa ´Alaa) katika Ubao uliohifadhiwa.
[1] Ahmad (1/307) na at-Tirmidhiy (2516) ambaye amesema:
”Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 117
Imechapishwa: 05/11/2024
https://firqatunnajia.com/105-hakubadilishwi-kitu-kilichoandikwa-katika-ubao-uliohifadhiwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
