Swali 102: Salaf wamewasema kwa ubaya wapiga visa. Ni upi mfumo wao? Tunatakiwa kuwa na msimamo upi juu yao?

Jibu: Salaf (Rahimahumu Allaah) wametahadharisha wapiga vita kwa sababu mara nyingi katika maneno yao wanajaribu kuwaathiri watu na visa ambapo havikusihi. Hawategemei dalili sahihi. Hawatilii uzito kuwafunza watu hukumu za dini na ´Aqiydah yao. Kwa sababu hawana uelewa. Leo wanawakilishwa na Jamaa´at-ut-Tabliygh na mfumo wao unaotambulika pamoja na ule usufi na ukhurafi walionao. Mara nyingi wapiga visa hutegemea maandiko ya makemeo ambapo wanawakatisha tamaa watu na rehema za Allaah (Ta´ala).

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Ajwibah al-Mufiydah ´an As-ilat-il-Manaahij al-Jadiydah, uk. 238-242
  • Imechapishwa: 13/08/2024
  • taaliki: Shaykh Jamaal bin Furahyaan al-Haarithiy