Katika Hadiyth hii kuna hukumu zifuatazo:
1 – Wajibu wa kufunga Ramadhaan.
2 – Kufunga Ramadhaan ni faradhi moja ya miongoni mwa faradhi za Uislamu.
3 – Ni nguzo ya pili kati ya nguzo za Uislamu. Allaah (Ta’ala) amesema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ
“Enyi mlioamini! Mmeandikiwa [fardhi ya] swawm kama ilivyoandikwa kwa walio kabla yenu mpate kumcha.”[1]
Kisha baada ya hapo akasema:
فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ
“Basi atakayeshuhudia miongoni mwenu mwezi [mpya] na afunge swawm.”[2]
Amri hii ni kwa njia ya ulazima. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Uislamu umejengwa juu ya mambo matano: kushuhudia kwamba hakuna mungu wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah, kusimamisha swalah, kutoa zakaah, kufunga Ramadhaan na kuhiji katika Nyumba tukufu ya Allaah.”[3]
[1] 02:183
[2] 02:185
[3] al-Bukhaariy (08) na Muslim (16).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Taysiyr Dhil-In´am bisharh ´Umdat-il-Ahkaam (01/437-438)
- Imechapishwa: 23/02/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)