Ni kuhusu yule swahabah aliyemwingilia mke wake mchana wa Ramadhaan. al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kupitia Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia ya kwamba kuna mtu alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kumwambia: “Ee Mtume wa Allaah! Nimeangamia.” Akamuuliza: “Ni kipi kimechokuangamiza?” Akajibu: “Nimemwingilia mke wangu [mchana wa] Ramadhaan ilihali nimefunga.”
Hii ni dhambi kubwa mtu akakusudia kumwingilia mke wake mchana wa Ramadhaan ilihali amefunga. Ni kipi alichomfanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam); alimshtua, alimtukana au alimkemea? Hapana. Kwa kuwa mwanaume huyu amekuja hali ya kuwa ni mwenye kutubia na kujuta. Si ambaye anapuuzia yale yaliyomtokea. Ndipo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamuuliza:
“Je, una mtumwa uwezaye kumwacha huru ikiwa ni kafara ya uliyofanya?” Akasema: “Hapana.” Akamuuliza: “Je, unaweza kufunga miezi miwili mfululizo?” Akasema: “Hapana.” Akamuuliza: “Je, unaweza kulisha masikini sitini?” Akasema: “Hapana.” Mtu yule akaketi chini. Tahamaki Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaja na tende na kumwambia: “Chukua hizi na uzitoe swadaqah.” Akamwambia: “Hivi kweli kuna fakiri uliko mimi, ee Mtume wa Allaah?” Ninaapa kwa Allaah! Hakuna kati ya nyumba hizi ambaye ni fakiri kuliko mimi.” Ndipo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akacheka mpaka yakaonekana magego yake. Halafu akasema: “Basi walishe familia yako.”
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Dawr-ul-Mar´ah fiy Iswlaah-il-Mujtama´ https://www.sahab.net/home/?p=806
- Imechapishwa: 02/02/2017
Ni kuhusu yule swahabah aliyemwingilia mke wake mchana wa Ramadhaan. al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kupitia Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia ya kwamba kuna mtu alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kumwambia: “Ee Mtume wa Allaah! Nimeangamia.” Akamuuliza: “Ni kipi kimechokuangamiza?” Akajibu: “Nimemwingilia mke wangu [mchana wa] Ramadhaan ilihali nimefunga.”
Hii ni dhambi kubwa mtu akakusudia kumwingilia mke wake mchana wa Ramadhaan ilihali amefunga. Ni kipi alichomfanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam); alimshtua, alimtukana au alimkemea? Hapana. Kwa kuwa mwanaume huyu amekuja hali ya kuwa ni mwenye kutubia na kujuta. Si ambaye anapuuzia yale yaliyomtokea. Ndipo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamuuliza:
“Je, una mtumwa uwezaye kumwacha huru ikiwa ni kafara ya uliyofanya?” Akasema: “Hapana.” Akamuuliza: “Je, unaweza kufunga miezi miwili mfululizo?” Akasema: “Hapana.” Akamuuliza: “Je, unaweza kulisha masikini sitini?” Akasema: “Hapana.” Mtu yule akaketi chini. Tahamaki Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaja na tende na kumwambia: “Chukua hizi na uzitoe swadaqah.” Akamwambia: “Hivi kweli kuna fakiri uliko mimi, ee Mtume wa Allaah?” Ninaapa kwa Allaah! Hakuna kati ya nyumba hizi ambaye ni fakiri kuliko mimi.” Ndipo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akacheka mpaka yakaonekana magego yake. Halafu akasema: “Basi walishe familia yako.”
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Dawr-ul-Mar´ah fiy Iswlaah-il-Mujtama´ https://www.sahab.net/home/?p=806
Imechapishwa: 02/02/2017
https://firqatunnajia.com/10-mfano-wa-pili-wa-hekima-ya-mtume-%d8%b5%d9%84%d9%89-%d8%a7%d9%84%d9%84%d9%87-%d8%b9%d9%84%d9%8a%d9%87-%d9%88%d8%b3%d9%84%d9%85/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)