Hadiyth ya tano
وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ ٌ
”Naye Yu pamoja nanyi popote mlipo.”[1]
مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَىٰ ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ
“Hauwi mnong’ono wa watatu isipokuwa Yeye ni wa nne wao.”[2]
43 – Abul-´Abbaas Ahmad bin ´Abdil-Hamiyd al-Maqdisiy ametukhabarisha: Abu Naswr Muusa bin ´Abdil-Qaadir al-Jiyliy ametuhadithia mwaka wa 618: ´Abdul-Awwal bin ´Iysaa as-Sijziy ametuhadithia: ´Abdur-Rahmaan bin Muhammad ad-Daawuudiy ametuhadithia: ´Abdullaah bin Hammuuyah as-Sarkhasiy ametuhadithia: Ibraahiym bin Khuzaym ash-Shaashiy ametuhadithia mwaka wa 316: ´Abd bin Humayd ametuhadithia: Habbaan bin Bilaal ametukhabarisha: Hammaam ametuhadithia: Thaabit ametuhadithia: Anas ametuhadithia ya kwamba Abu Bakr as-Swiddiyq alisema akumwambia:
”Wakati tulipokuwa ndani ya pango nilitazama miguu ya washirikina. Nikasema: ”Ee Mtume wa Allaah! Lau mmoja wao angelitazama miguu yake kwa chini basi angelituona.” Akasema: ”Ee Abu Bakr! Unafikiriaje wawili ambao Allaah ndiye watatu wao?”[3]
Ameipokea Muslim kupitia kwa ´Abd bin Humayd.
44 – Watu wa tafsiri, akiwemo adh-Dhwahhaak, wamesema kuhusu maneno Yake (Ta´ala):
مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَىٰ ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ
“Hauwi mnong’ono wa watatu isipokuwa Yeye ni wa nne wao.”[4]
”Yuko juu ya ´Arshi na utambuzi Wake uko pamoja nao.”
45 – Maalik amesema:
”Allaah yuko juu ya mbingu na ujuzi Wake uko kila mahali.”
46 – Sufyaan amesema kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):
وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ ٌ
”Naye Yu pamoja nanyi popote mlipo.”
”Bi maana ujuzi Wake.”[5]
47 – Muqaatil bin Hayyaan amesema maneno Yake Allaah (Ta´ala):
مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَىٰ ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ
“Hauwi mnong’ono wa watatu isipokuwa Yeye ni wa nne wao.”
”Yuko (Ta´ala) juu ya ´Arshi na ujuzi Wake uko pamoja nao.”[6]
Amesema (Rahimahu Allaah) kuhusu ukaribu wa Allaah:
”Bi maana kwa ujuzi Wake na wakati huohuo Yuko juu ya ´Arshi Yake.”[7]
48 – Wakati Nu´aym bin Hammaad, mwalimu wake na al-Bukhaariy, alipoulizwa kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):
وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ ٌ
”Naye Yu pamoja nanyi popote mlipo.”[8]
akasema:
”Maana yake ni kwamba hakuna chochote kile kinachojficha Kwake.”
[1] 57:4
[2] 58:7
[3] Muslim (2381).
[4] 58:7
[5] Kitaab-us-Sunnah, uk. 187-189
[6] Sharh Usuwl I´tiqaad Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah (3/387-402).
[7] al-Asmaa’ was-Swifaat, uk. 542, ya al-Bayhaqiy.
[8] 57:4
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 61-64
- Imechapishwa: 02/06/2024
Hadiyth ya tano
وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ ٌ
”Naye Yu pamoja nanyi popote mlipo.”[1]
مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَىٰ ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ
“Hauwi mnong’ono wa watatu isipokuwa Yeye ni wa nne wao.”[2]
43 – Abul-´Abbaas Ahmad bin ´Abdil-Hamiyd al-Maqdisiy ametukhabarisha: Abu Naswr Muusa bin ´Abdil-Qaadir al-Jiyliy ametuhadithia mwaka wa 618: ´Abdul-Awwal bin ´Iysaa as-Sijziy ametuhadithia: ´Abdur-Rahmaan bin Muhammad ad-Daawuudiy ametuhadithia: ´Abdullaah bin Hammuuyah as-Sarkhasiy ametuhadithia: Ibraahiym bin Khuzaym ash-Shaashiy ametuhadithia mwaka wa 316: ´Abd bin Humayd ametuhadithia: Habbaan bin Bilaal ametukhabarisha: Hammaam ametuhadithia: Thaabit ametuhadithia: Anas ametuhadithia ya kwamba Abu Bakr as-Swiddiyq alisema akumwambia:
”Wakati tulipokuwa ndani ya pango nilitazama miguu ya washirikina. Nikasema: ”Ee Mtume wa Allaah! Lau mmoja wao angelitazama miguu yake kwa chini basi angelituona.” Akasema: ”Ee Abu Bakr! Unafikiriaje wawili ambao Allaah ndiye watatu wao?”[3]
Ameipokea Muslim kupitia kwa ´Abd bin Humayd.
44 – Watu wa tafsiri, akiwemo adh-Dhwahhaak, wamesema kuhusu maneno Yake (Ta´ala):
مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَىٰ ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ
“Hauwi mnong’ono wa watatu isipokuwa Yeye ni wa nne wao.”[4]
”Yuko juu ya ´Arshi na utambuzi Wake uko pamoja nao.”
45 – Maalik amesema:
”Allaah yuko juu ya mbingu na ujuzi Wake uko kila mahali.”
46 – Sufyaan amesema kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):
وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ ٌ
”Naye Yu pamoja nanyi popote mlipo.”
”Bi maana ujuzi Wake.”[5]
47 – Muqaatil bin Hayyaan amesema maneno Yake Allaah (Ta´ala):
مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَىٰ ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ
“Hauwi mnong’ono wa watatu isipokuwa Yeye ni wa nne wao.”
”Yuko (Ta´ala) juu ya ´Arshi na ujuzi Wake uko pamoja nao.”[6]
Amesema (Rahimahu Allaah) kuhusu ukaribu wa Allaah:
”Bi maana kwa ujuzi Wake na wakati huohuo Yuko juu ya ´Arshi Yake.”[7]
48 – Wakati Nu´aym bin Hammaad, mwalimu wake na al-Bukhaariy, alipoulizwa kuhusu maneno Yake Allaah (Ta´ala):
وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ ٌ
”Naye Yu pamoja nanyi popote mlipo.”[8]
akasema:
”Maana yake ni kwamba hakuna chochote kile kinachojficha Kwake.”
[1] 57:4
[2] 58:7
[3] Muslim (2381).
[4] 58:7
[5] Kitaab-us-Sunnah, uk. 187-189
[6] Sharh Usuwl I´tiqaad Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah (3/387-402).
[7] al-Asmaa’ was-Swifaat, uk. 542, ya al-Bayhaqiy.
[8] 57:4
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 61-64
Imechapishwa: 02/06/2024
https://firqatunnajia.com/10-hadiyth-unafikiriaje-wawili-ambao-allaah-ndiye-watatu-wao/