60 – Kwa njia hiyohiyo ametuhadithia Sulaymaan bin Harb, kutoka kwa Hammaad bin Zayd, ambaye amesema:
”Ayyuub alinikabidhi nguo akasema: “Nikatie iwe kama kanzu. Uweke sehemu ya mwisho ya mkono wake kuwa shibri na uifanye iingie hadi juu ya kisigino.”
61 – Ishaaq bin Ibraahiym ametuhadithia, kutoka kwa ´Abdur-Razzaaq, kutoka kwa Ma´mar, ambaye amesema:
”Nilimkosoa Ayyuub juu ya urefu wa kanzu yake, akasema: “Hakika umaarufu zamani ulikuwa katika urefu wake, lakini leo ni katika kuikunja.”
62 – Muhammad bin Sallaam al-Jumahiy ametuhadithia: ´Adiy bin al-Fadhwl ametuhadithia: Ayyuub amenambia:
“Tengeneza viatu viwili kwa namna ya mfano wa viatu vya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).” Nikafanya hivyo. Akavivaa kwa siku kadhaa kisha akaviacha. Nikamuuliza kuhusu hilo, akasema: “Sikuona watu wakivivaa.”
63 – ´Aliy bin al-Ja´d ametuhadithia: Qays bin ar-Rabiy´ ametukhabarisha, kutoka kwa Mansuur, kutoka kwa Ibraahiym, ambaye amesema:
“Usivae katika nguo kile ambacho wanavyuoni watakujua kwa sababu yake wala wajinga wakakudharau kwa sababu yake.”
64 – al-Hakam bin Muusa ametuhadithia: Ghassaan bin ´Ubayd ametuhadithia, kutoka kwa Sufyaan ath-Thawriy, ambaye amesema:
“Walikuwa wanachukia aina mbili za umaarufu: nguo nzuri sana ambazo mtu anajulikana nazo na watu wanainua macho yao kumwangalia kwa sababu yake, na nguo mbaya sana ambazo mtu anadharauliwa na dini yake kudhalilishwa.”
65 – Khaalid bin Khidaash ametuhadithia: Hammaad bin Zayd ametuhadithia, kutoka kwa Abu Khushaynah, swahiba yake az-Ziyaadiy, aliyesema:
”Siku moja tulikuwa pamoja na Abu Qilaabah wakati alipoingia bwana mmoja ambaye alikuwa amevaa mashuka. Akasema: “Jihadharini na huyu punda mpiga kelele.”
66 – Khalaf bin Hishaam ametuhadithia: Hammaad bin Zayd ametuhadithia, kutoka kwa bwana mmoja, kutoka kwa Abu Bakr, kutoka kwa al-Hasan, ambaye amesema:
“Hakika kuna watu ambao wamefanya kiburi kuwa katika mioyo yao na unyenyekevu katika nguo zao. Hivyo basi mwenye joho la kawaida amejivuna zaidi kuliko mwenye joho la kifakhari – muda wa kuwa hawajifanyi kuwa ni mafukara.”
67 – Abu Ishaaq Ismaa´iyl bin al-Haarith ametuhadithia:: Muhammad bin Muqaatil ametuhadithia: Ibn-ul-Mubaarak ametuhadithia: Abu ´Awaanah ametuhadithia, kutoka kwa Sulaymaan ash-Shaybaaniy: Bwana mmoja ametuhadithia:
”Ibn ´Umar alimuona mwanawe amevaa kanzu mbaya na ya hali ya chini, akasema: “Usivae hii. Hakika hii ni kanzu ya umaarufu.”
- Muhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiyd-Dunyaa (afk. 281)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-ul-Khumuul wat-Tawaadhwu´, uk. 84-91
- Imechapishwa: 29/01/2026
60 – Kwa njia hiyohiyo ametuhadithia Sulaymaan bin Harb, kutoka kwa Hammaad bin Zayd, ambaye amesema:
”Ayyuub alinikabidhi nguo akasema: “Nikatie iwe kama kanzu. Uweke sehemu ya mwisho ya mkono wake kuwa shibri na uifanye iingie hadi juu ya kisigino.”
61 – Ishaaq bin Ibraahiym ametuhadithia, kutoka kwa ´Abdur-Razzaaq, kutoka kwa Ma´mar, ambaye amesema:
”Nilimkosoa Ayyuub juu ya urefu wa kanzu yake, akasema: “Hakika umaarufu zamani ulikuwa katika urefu wake, lakini leo ni katika kuikunja.”
62 – Muhammad bin Sallaam al-Jumahiy ametuhadithia: ´Adiy bin al-Fadhwl ametuhadithia: Ayyuub amenambia:
“Tengeneza viatu viwili kwa namna ya mfano wa viatu vya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).” Nikafanya hivyo. Akavivaa kwa siku kadhaa kisha akaviacha. Nikamuuliza kuhusu hilo, akasema: “Sikuona watu wakivivaa.”
63 – ´Aliy bin al-Ja´d ametuhadithia: Qays bin ar-Rabiy´ ametukhabarisha, kutoka kwa Mansuur, kutoka kwa Ibraahiym, ambaye amesema:
“Usivae katika nguo kile ambacho wanavyuoni watakujua kwa sababu yake wala wajinga wakakudharau kwa sababu yake.”
64 – al-Hakam bin Muusa ametuhadithia: Ghassaan bin ´Ubayd ametuhadithia, kutoka kwa Sufyaan ath-Thawriy, ambaye amesema:
“Walikuwa wanachukia aina mbili za umaarufu: nguo nzuri sana ambazo mtu anajulikana nazo na watu wanainua macho yao kumwangalia kwa sababu yake, na nguo mbaya sana ambazo mtu anadharauliwa na dini yake kudhalilishwa.”
65 – Khaalid bin Khidaash ametuhadithia: Hammaad bin Zayd ametuhadithia, kutoka kwa Abu Khushaynah, swahiba yake az-Ziyaadiy, aliyesema:
”Siku moja tulikuwa pamoja na Abu Qilaabah wakati alipoingia bwana mmoja ambaye alikuwa amevaa mashuka. Akasema: “Jihadharini na huyu punda mpiga kelele.”
66 – Khalaf bin Hishaam ametuhadithia: Hammaad bin Zayd ametuhadithia, kutoka kwa bwana mmoja, kutoka kwa Abu Bakr, kutoka kwa al-Hasan, ambaye amesema:
“Hakika kuna watu ambao wamefanya kiburi kuwa katika mioyo yao na unyenyekevu katika nguo zao. Hivyo basi mwenye joho la kawaida amejivuna zaidi kuliko mwenye joho la kifakhari – muda wa kuwa hawajifanyi kuwa ni mafukara.”
67 – Abu Ishaaq Ismaa´iyl bin al-Haarith ametuhadithia:: Muhammad bin Muqaatil ametuhadithia: Ibn-ul-Mubaarak ametuhadithia: Abu ´Awaanah ametuhadithia, kutoka kwa Sulaymaan ash-Shaybaaniy: Bwana mmoja ametuhadithia:
”Ibn ´Umar alimuona mwanawe amevaa kanzu mbaya na ya hali ya chini, akasema: “Usivae hii. Hakika hii ni kanzu ya umaarufu.”
Muhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiyd-Dunyaa (afk. 281)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Kitaab-ul-Khumuul wat-Tawaadhwu´, uk. 84-91
Imechapishwa: 29/01/2026
https://firqatunnajia.com/09-jihadhari-na-mavazi-ya-umaarufu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket