1 – Imaam an-Nawawiy amesema katika “al-Majmuu´” kuhusu kupaka hina:
“Kuhusu kupaka hina mikononi na miguuni ni jambo limependekezwa kwa wanawake walioolewa kutokana na Hadiyth zilizotangaa juu yake.”[1]
Anaashiria yale yaliyopokelewa na Abu Daawuud ya kwamba kuna mwanamke alimuuliza ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) kuhusu upakaji hina ambapo akajibu:
“Hakuna neno. Lakini hata hivyo mimi nalichukia. Hakika mpenzi wangu Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akichukia harufu yake.”
Ameipokea an-Nasaa´iy.
´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia:
“Mwanamke mmoja alimuashiria Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) nyuma ya pazia kitabu ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akakamata mkono wake na akasema: “Sijui ni mkono wa mwanaume au mkono wa mwanamke?” Akasema: “Ni mkono wa mwanamke.” Akasema: “Ungelikuwa ni mwanamke basi ungelibadilisha [rangi] kucha zako.”
Bi maana kuzibadilisha kwa hina.
Ameipokea Abu Daawuud na an-Nasaa´iy.
Lakini asipake rangi kucha zake kwa rangi ambayo inamganda na kuzuia twahara yake.
[1] (01/324).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 22-23
- Imechapishwa: 23/10/2019
1 – Imaam an-Nawawiy amesema katika “al-Majmuu´” kuhusu kupaka hina:
“Kuhusu kupaka hina mikononi na miguuni ni jambo limependekezwa kwa wanawake walioolewa kutokana na Hadiyth zilizotangaa juu yake.”[1]
Anaashiria yale yaliyopokelewa na Abu Daawuud ya kwamba kuna mwanamke alimuuliza ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) kuhusu upakaji hina ambapo akajibu:
“Hakuna neno. Lakini hata hivyo mimi nalichukia. Hakika mpenzi wangu Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akichukia harufu yake.”
Ameipokea an-Nasaa´iy.
´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia:
“Mwanamke mmoja alimuashiria Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) nyuma ya pazia kitabu ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akakamata mkono wake na akasema: “Sijui ni mkono wa mwanaume au mkono wa mwanamke?” Akasema: “Ni mkono wa mwanamke.” Akasema: “Ungelikuwa ni mwanamke basi ungelibadilisha [rangi] kucha zako.”
Bi maana kuzibadilisha kwa hina.
Ameipokea Abu Daawuud na an-Nasaa´iy.
Lakini asipake rangi kucha zake kwa rangi ambayo inamganda na kuzuia twahara yake.
[1] (01/324).
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 22-23
Imechapishwa: 23/10/2019
https://firqatunnajia.com/09-hukumu-ya-mwanamke-kupaka-hina/