36 – Imesihi kwamba Qataadah amesema:
”Wana wa israaiyl walikuwa wakisema: ”Ee Mola! Wewe uko juu ya mbingu na sisi tuko ardhini. Ni vipi tutajua kuwa umeridhia au umeghadhibika?” Akasema: ”Ninapokuwa radhi nanyi basi Hufanya wale wabora wenu ndio wakakutawaleni na ninapokughadhibikieni basi Hufanya wale waovu wenu ndio wakakutawaleni.”
37 – Imethibiti kwamba Thaabit al-Bunaaniy amesema:
”Daawuud alikuwa akirefusha swalah, kisha akirukuu, kisha akiinua kichwa juu mbinguni kisha akisema: ”Ee Ambaye uko juu ya mbingu. Nimekiinua kichwa Changu kukuelekea, kama ambavo watumwa wanawatazama mabwana wao, Ee Ambaye unaishi juu ya mbingu!”[1]
38 – Abu Haniyfah amesema:
”Anayepinga kwamba Allaah (Ta´ala) yuko juu ya mbingu amekufuru.”
39 – Maalik amesema:
”Allaah yuko juu ya mbingu na ujuzi Wake uko kila mahali – hakuna kinachojificha Kwake.”[2]
40 – Hammaad bin Zayd amesema kuhusu Jahmiyyah:
”Wanachotaka kusema ni kuwa hakuna mungu yeyote juu ya mbingu.”
41 – Jariyr bin ´Abdil-Hamiyd amesema:
”Maneno ya Jahmiyyah mwanzo wake ni asali na mwisho wake ni sumu. Mambo yalivyo ni kwamba wanachotaka kusema ni kwamba hakuna mungu yeyote juu ya mbingu.”
42 – Bwana mmoja alisema kumwambia Ibn-ul-Mubaarak:
”Ee Abu ´Abdir-Rahmaan! Namukhofu Allaah (´Azza wa Jall) kutokana na wingi nilivyomuomba Allaah dhidi ya Jahmiyyah.” Akasema: ”Usikhofu. Kwani wao wanadai kuwa mungu wako aliye juu ya mbingu si chochote.”
[1] adh-Dhahabiy amesema:
”Cheni ya wapokezi wake ni salama.” (al-´Uluww, uk. 552)
[2] al-Laalakaa’iy (2/401), ´Abdullaah bin Ahmad katika ”as-Sunnah” (1/107) na al-Aajurriy katika ”ash-Shariy´ah”, uk. 289.
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 58-60
- Imechapishwa: 02/06/2024
36 – Imesihi kwamba Qataadah amesema:
”Wana wa israaiyl walikuwa wakisema: ”Ee Mola! Wewe uko juu ya mbingu na sisi tuko ardhini. Ni vipi tutajua kuwa umeridhia au umeghadhibika?” Akasema: ”Ninapokuwa radhi nanyi basi Hufanya wale wabora wenu ndio wakakutawaleni na ninapokughadhibikieni basi Hufanya wale waovu wenu ndio wakakutawaleni.”
37 – Imethibiti kwamba Thaabit al-Bunaaniy amesema:
”Daawuud alikuwa akirefusha swalah, kisha akirukuu, kisha akiinua kichwa juu mbinguni kisha akisema: ”Ee Ambaye uko juu ya mbingu. Nimekiinua kichwa Changu kukuelekea, kama ambavo watumwa wanawatazama mabwana wao, Ee Ambaye unaishi juu ya mbingu!”[1]
38 – Abu Haniyfah amesema:
”Anayepinga kwamba Allaah (Ta´ala) yuko juu ya mbingu amekufuru.”
39 – Maalik amesema:
”Allaah yuko juu ya mbingu na ujuzi Wake uko kila mahali – hakuna kinachojificha Kwake.”[2]
40 – Hammaad bin Zayd amesema kuhusu Jahmiyyah:
”Wanachotaka kusema ni kuwa hakuna mungu yeyote juu ya mbingu.”
41 – Jariyr bin ´Abdil-Hamiyd amesema:
”Maneno ya Jahmiyyah mwanzo wake ni asali na mwisho wake ni sumu. Mambo yalivyo ni kwamba wanachotaka kusema ni kwamba hakuna mungu yeyote juu ya mbingu.”
42 – Bwana mmoja alisema kumwambia Ibn-ul-Mubaarak:
”Ee Abu ´Abdir-Rahmaan! Namukhofu Allaah (´Azza wa Jall) kutokana na wingi nilivyomuomba Allaah dhidi ya Jahmiyyah.” Akasema: ”Usikhofu. Kwani wao wanadai kuwa mungu wako aliye juu ya mbingu si chochote.”
[1] adh-Dhahabiy amesema:
”Cheni ya wapokezi wake ni salama.” (al-´Uluww, uk. 552)
[2] al-Laalakaa’iy (2/401), ´Abdullaah bin Ahmad katika ”as-Sunnah” (1/107) na al-Aajurriy katika ”ash-Shariy´ah”, uk. 289.
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 58-60
Imechapishwa: 02/06/2024
https://firqatunnajia.com/09-allaah-yuko-juu-ya-mbingu-na-sisi-tuko-ardhini/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
