Matukio yaliyotokea kwa yule ambaye ndiye kiumbe aliye na hekima zaidi yanafahamisha kutumia hekima wakati wa kulingania katika dini ya Allaah. Naye si mwengine ni Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hebu wacha tupige mifano juu ya hilo.
Mfano wa kwanza: Ni yule mbedui aliyekojoa msikitini.
al-Bukhaariy na Muslim na wengineo wamepokea kupitia kwa Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia ya kwamba kuna mbedui aliyeingia msikitini na akatafuta pembe msikitini kisha akaanza kukojoa. Maswahabah wakapanda juu, wakamkataza na kumfokea. Lakini Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye Allaah amempa hekima ya kulingania katika dini Yake (´Azza wa Jall) akawakataza kumfokea na akawaambia:
“Msimkatikize.”
Bi maana msimkatikize mkojo wake. Pindi mbedui yule alipomaliza kukojoa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaamrisha wamwage ndoo ya maji juu ya ule mkojo. Baada ya hapo akamwita yule mbedui na kumwambia:
“Misikiti hii haisilihi ndani yake kitu katika dhara na taka. Imewekwa kwa ajili ya swalah, kusoma Qur-aan na kumdhukuru Allaah (´Azza wa Jall).”
Au alisema maneno mfano wa hayo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) amepokea kuwa mbedui huu alisema:
“Ee Allaah! Nihurumie mimi na Muhammad na usimuhurumie kati yetu mwengine yeyote.”
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Dawr-ul-Mar´ah fiy Iswlaah-il-Mujtama´ https://www.sahab.net/home/?p=806
- Imechapishwa: 02/02/2017
Matukio yaliyotokea kwa yule ambaye ndiye kiumbe aliye na hekima zaidi yanafahamisha kutumia hekima wakati wa kulingania katika dini ya Allaah. Naye si mwengine ni Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hebu wacha tupige mifano juu ya hilo.
Mfano wa kwanza: Ni yule mbedui aliyekojoa msikitini.
al-Bukhaariy na Muslim na wengineo wamepokea kupitia kwa Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia ya kwamba kuna mbedui aliyeingia msikitini na akatafuta pembe msikitini kisha akaanza kukojoa. Maswahabah wakapanda juu, wakamkataza na kumfokea. Lakini Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye Allaah amempa hekima ya kulingania katika dini Yake (´Azza wa Jall) akawakataza kumfokea na akawaambia:
“Msimkatikize.”
Bi maana msimkatikize mkojo wake. Pindi mbedui yule alipomaliza kukojoa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaamrisha wamwage ndoo ya maji juu ya ule mkojo. Baada ya hapo akamwita yule mbedui na kumwambia:
“Misikiti hii haisilihi ndani yake kitu katika dhara na taka. Imewekwa kwa ajili ya swalah, kusoma Qur-aan na kumdhukuru Allaah (´Azza wa Jall).”
Au alisema maneno mfano wa hayo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) amepokea kuwa mbedui huu alisema:
“Ee Allaah! Nihurumie mimi na Muhammad na usimuhurumie kati yetu mwengine yeyote.”
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Dawr-ul-Mar´ah fiy Iswlaah-il-Mujtama´ https://www.sahab.net/home/?p=806
Imechapishwa: 02/02/2017
https://firqatunnajia.com/08-mfano-wa-kwanza-wa-hekima-ya-mtume-%d8%b5%d9%84%d9%89-%d8%a7%d9%84%d9%84%d9%87-%d8%b9%d9%84%d9%8a%d9%87-%d9%88%d8%b3%d9%84%d9%85/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)