08 – Kuomba msamah. Amesema (Ta´ala):

فَاعْلَمْ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا اللَّـهُ وَاسْتَغْفِرْ لِذَنبِكَ

“Basi elewa kwamba hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah na omba msamaha kwa dhambi zako.”[1]

Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

”Yule mwenye kulazimiana na kuomba msamaha basi Allaah atamfanyia njia ya kutokea katika kila dhiki, faraja juu ya kila simanzi na atamruzuku kwa njia asiyoitarajia.”[2]

Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika yale aliyopokea kutoka kwa Mola wake:

Ee mwanaadamu! Lau madhambi yako yangelifika kwenye mawingu ya mbingu kisha ukaniomba msamaha basi Ningelikusamehe.”[3]

Haya, ee dada wa Kiislamu, ndio bora ambayo unaweza kutumia muda wako. Hivyo basi, fanya hivo kwa wingi ili moyo wako uweze kupata utulivu. Amesema (Ta´ala):

أَلَا بِذِكْرِ اللَّـهِ تَطْمَئِنُّ الْقُلُوبُ

“Zindukeni! Kwa kumtaja Allaah nyoyo hutulia!”[4]

[1] 47:19

[2] Abu Daawuud na Ibn Maajah. Ni dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Dhwa´iyf-ul-Jaamiy´”, uk. 841 nr. 5829.

[3] at-Tirmidhiy (05/548) nr. 3540 ambaye amesema:

”Hadiyth hii ni ngeni. Hatuitambui isipokuwa kwa njia hii.”

[4] 13:28

  • Muhusika: Dr. ´Abdul-´Aziyz bin Daawuud al-Faaiz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tawjiyhaat wa Tanbiyhaat lil-Fataati al-Muslimah, uk. 17
  • Imechapishwa: 09/02/2026