08. Hadiyth ”Yule mwenye kuniswalia mara moja… ”

8 – Abu Thaabit ametuhadithia: ´Abdul-´Aziyz bin Abiy Haazim ametuhadithia, kutoka kwa al-´Alâ’ bin ´Abdir-Rahmaan, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Abu Hurayrah, ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

من صلَّى عليَّ صلى الله عليه عشراً

”Yule mwenye kuniswalia mara moja, basi Allaah atamswalia mara kumi.”[1]

[1] Cheni ya wapokezi wake ni Swahiyh. Wanamme wake ni wanamme Swahiyh. Abu Thaabit anaitwa Muhammad bin ´Ubaydillaah bin Muhammad al-Madaniy. Kisha imesimuliwa kupitia njia nyingine kutoka kwa al-´Alaa na njia nyingine ya tatu (11).

  • Muhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Ishaaq al-Maalikiy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy, uk. 28
  • Imechapishwa: 15/03/2023
  • Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy