وإذا قيل لك : من نبيك؟

Swali 6: Ni nani Mtume wako?

نبينا محمد بن عبد الله بن عبد المطلب بن هاشم بن عبد مناف

Jibu: Mtume wetu ni Muhammad bin ´Abdillaah bin ´Abdil-Muttwalib bin Haashim bin ´Abdil-Manaaf.

اصطفاه الله تعالى من قريش وهم صفوة ولد إسماعيل، وبعثه إلى الأحمر والأسود، وأنزل عليه الكتاب والحكمة تدعي الناس إلى إخلاص العبادة و ترك ما كانوا يعبدون من دون الله من : الأصنام – الأحجار- والأشجار، والأنبياء، والصالحين، والملائكة، وغيره

Allaah (Ta´ala) amemteua kutoka kwa Quraysh. Quraysh ndio kabila bora kutoka katika kizazi cha Ismaa´iyl. Allaah amemtuma Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa watu weupe na weusi. Allaah amemteremshia Kitabu na hekima. Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akawalingania watu katika kumuabudu Allaah peke yake na kuacha vyenginevyo walivyokuwa wakiviabudu badala ya Allaah katika masanamu, miti, manabii, watu wema, malaika na vyenginevyo.

فدعى الناس إلى ترك الشرك وقاتلهم إلى تركه وأن تخلصوا لعبادة الله كمال قال تعالى

Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akawalingania watu katika kujiepusha na shirki. Akawapiga vita ili waache shirki na badala yake wamuabudu Allaah peke yake. Allaah (Ta´ala) amesema:

قُلْ إِنَّمَا أَدْعُو رَبِّي وَلَا أُشْرِكُ بِهِ أَحَدًا

“Sema: “Hakika mimi namuomba Mola wangu Pekee na wala simshirikishi na yeyote.”[1]

قُلِ اللَّـهَ أَعْبُدُ مُخْلِصًا لَّهُ دِينِي

“Sema: “Allaah Pekee namwambudu nikimtakasia Dini yangu kwa ajili Yake.”[2]

قُلْ إِنَّمَا أُمِرْتُ أَنْ أَعْبُدَ اللَّـهَ وَلَا أُشْرِكَ بِهِ ۚ إِلَيْهِ أَدْعُو وَإِلَيْهِ مَآبِ

“Sema: “Hakika mimi nimeamrishwa nimwabudu Allaah na nisimshirikishe na chochote. Kwake nalingania na Kwake ni marejeo yangu.”[3]

قُلْ أَفَغَيْرَ اللَّـهِ تَأْمُرُونِّي أَعْبُدُ أَيُّهَا الْجَاهِلُونَ وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ بَلِ اللَّـهَ فَاعْبُدْ وَكُن مِّنَ الشَّاكِرِينَ

“Sema: “Je, mnaniamrisha nimuabudu asiyekuwa Allaah enyi majahili?” Kwa yakini umefunuliwa Wahy na kwa wale walio kabla yako kwamba: Ukifanya shirki bila shaka zitaporomoka ‘amali zako na bila shaka [Aakhirah] utakuwa miongoni mwa waliokhasirika. Bali Allaah Pekee mwabudu na uwe miongoni mwa wenye kushukuru.”[4]

[1] 72:20

[2] 39:14

[3] 13:36

[4] 39:64-66

  • Mhusika: Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ta´liym-us-Swibyaan at-Tawhiyd, uk. 22-25
  • Imechapishwa: 25/03/2017