12- Kwa wale ambao Miyqaat yao ni Dhul- Hulayfah basi imependezwa kwao kuswali hapo. Swalah hii sio kwa sababu ya umaalum wa Ihraam, bali ni kwa sababu ya sifa maalum ya mahali na baraka. al-Bukhaariy amepokea kutoka kwa ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) akisimulia kwamba amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema kwenye bonde la ´Aqiyq:
“Wakati wa usiku amenijia mimi mwenye kuja kutoka kwa Mola wangu na akasema: “Swali katika bonde hili lenye kubarikiwa na akasema: “´Umrah – na katika upokezi mwingine “´Umrah na hajj.””
Ibn ´Umar ameeleza kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyesema:
“Alionekana na hali ya kuwa ni mwenye kuteremka wakati wa usiku kwa ajili ya kupumzika hapo Dhul-Hulayfah katikati ya bonde. Akaambiwa: “Hakika wewe uko katika Batwhaa´ lililobarikiwa.””[1]
[1] Tazama “Swahiyh Abiy Daawuud” (1579) na “Mukhtaswar Swahiyh Muslim” (761-762) – Allaah asahilishe chapisho lake. Haafidhw amesema:
“Katika Hadiyth tunapata kufahamu kwmaba fadhilah za ´Aqiyq ni kama fadhilah za al-Madiynah na fadhilah za kuswali hapo… ” (Fath-ul-Baariy (3/311))
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Manaasik-ul-Hajj wal-´Umrah, uk. 16
- Imechapishwa: 06/07/2018
12- Kwa wale ambao Miyqaat yao ni Dhul- Hulayfah basi imependezwa kwao kuswali hapo. Swalah hii sio kwa sababu ya umaalum wa Ihraam, bali ni kwa sababu ya sifa maalum ya mahali na baraka. al-Bukhaariy amepokea kutoka kwa ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) akisimulia kwamba amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema kwenye bonde la ´Aqiyq:
“Wakati wa usiku amenijia mimi mwenye kuja kutoka kwa Mola wangu na akasema: “Swali katika bonde hili lenye kubarikiwa na akasema: “´Umrah – na katika upokezi mwingine “´Umrah na hajj.””
Ibn ´Umar ameeleza kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyesema:
“Alionekana na hali ya kuwa ni mwenye kuteremka wakati wa usiku kwa ajili ya kupumzika hapo Dhul-Hulayfah katikati ya bonde. Akaambiwa: “Hakika wewe uko katika Batwhaa´ lililobarikiwa.””[1]
[1] Tazama “Swahiyh Abiy Daawuud” (1579) na “Mukhtaswar Swahiyh Muslim” (761-762) – Allaah asahilishe chapisho lake. Haafidhw amesema:
“Katika Hadiyth tunapata kufahamu kwmaba fadhilah za ´Aqiyq ni kama fadhilah za al-Madiynah na fadhilah za kuswali hapo… ” (Fath-ul-Baariy (3/311))
Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Manaasik-ul-Hajj wal-´Umrah, uk. 16
Imechapishwa: 06/07/2018
https://firqatunnajia.com/07-kuswali-katika-bonde-la-aqiyq/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)