6- Abu Hurayrah amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mkono wa kuume wa Allaah (´Azza wa Jall) umejaa. Haupungui kitu kwa kutoa mchana na usiku. Kwenye mkono Wake mwengine kuna mizani ambayo anapandisha na anashusha.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariu na Muslim.
[1] al-Bukhaariy (4684), Muslim (993), Ahmad (2/242) na at-Tirmidhiy (3045) aliyesema:
“Hadiyth hii ni nzuri na Swahiyh na inafasiri Aayah isemayo:
وَقَالَتِ الْيَهُودُ يَدُ اللَّـهِ مَغْلُولَةٌ ۚ غُلَّتْ أَيْدِيهِمْ وَلُعِنُوا بِمَا قَالُوا ۘ بَلْ يَدَاهُ مَبْسُوطَتَانِ يُنفِقُ كَيْفَ يَشَاءُ
“Mayahudi wakasema: “Mkono wa Allaah imefumbwa”. Mikono yao ndio iliyofumbwa na wamelaaniwa kwa yale waliyoyasema. Bali mikono Yake imekunjuliwa hutoa atakavyo.” (05:64)
Hadiyth imepokelewa na maimamu. Tunaiamini kama ilivyokuja pasi na kuipindisha wala kuifanyia namna. Hivo ndivo walivosema maimamu akiwemo Sufyaan ath-Thawriy, Maalik bin Anas, Ibn ´Uyaynah na Ibn-ul-Mubaarak; zinatakiwia kusimiliwa na kuziamin pasi na kuzifanyia namna.”
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ithbaat-ul-Yad li-Laah Swifatan min Swifwaatih, uk. 18
- Imechapishwa: 17/06/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)