30 – Ahmad bin ´Iysaa al-Miswriy amenihadithia: ´Abdullaah bin Wahb ametuhadithia, kutoka kwa ´Amr bin al-Haarith na Ibn Lahiy´ah, kutoka kwa Yaziyd bin Abiy Habiyb, kutoka kwa Sinaan bin Sa´d, kutoka kwa Anas bin Maalik, kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), ambaye amesema:
“Inatosha kuoneysha uovu wa mtu, isipokuwa yule ambaye amekingwa na (´Azza wa Jall), kuwa watu wamuelekezea vidole katika dini yake na dunia yake.”
31 – Ishaaq bin al-Bahluul at-Tanuukhiy ametuhadithia: Ibn Abiy Fudayk ametuhadithia: Muhammad bin Sulaymaan al-Akhnasiy ametuhadithia, kutoka kwa ´Abdul-Waahid bin Abiy Kathiyr, kutoka kwa Jaabir bin ´Abdillaah, ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Inatosha kuoneysha uovu wa mtu, isipokuwa yule ambaye amekingwa na (´Azza wa Jall), kuwa watu wamuelekezea vidole katika dini yake na dunia yake. Hakika Allaah hatazami sura zenu; lakini anazitazama nyoyo na matendo yenu.”
32 – ´Aliy bin al-Ja´d ametuhadithia: al-Mubaarak bin Fadhwaalah ametukhabarisha, kutoka kwa al-Hasan, aliyeeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Inatosha kuoneysha uovu wa mtu watu wanamuelekezea vidole katika dini yake na dunia yake.”
33 – Abun-Naswr al-Mu-addib amenihadithia: Daawuud bin al-Muhabbir ametuhadithia, kutoka kwa al-Mubaarak bin Fadhwaalah, ambaye amesema:
”Tulimwambia al-Hasan: ”Ee Abu Sa´iyd, hakika watu wakikuona wanakuashiria kwa vidole.” Akasema: ”Si hicho kilichokusudiwa hapa. Hakika hapana vyenginevyo kilichoksudiwa ni mzushi katika dini yake na fasiki katika dunia yake.”
34 – Baba yangu amenihadithia: Ibraahiym bin Hiraasah ametuhadithia, kutoka kwa al-Quraah, kutoka kwa mzee mmoja kutoka Ahnaf, ambaye ameeleza kuwa amemsikia ´Aliy akisema:
“Jidunike, acha kujulikana. Usijiinue mwenyewe ukatajwa na hivyo ukatambulika. Kithirisha kukaa kimya utasalimika, wafurahishe wema na wachukize waovu.”
35 – Ahmad bin Ibraahiym ametuhadithia: Ahmad bin Kurduus ametuhadithia: Makhlad bin al-Husayn ametuhadithia, kutoka kwa Abu Bakr bin al-Fadhwl: Nimemsikia Ayyuub akisema:
“Hakuna hatokuwa mkweli na Allaah isipokuwa hufurahi asijulikane mahali alipo.”
36 – Kwa njia hiyohiyo ametuhadithia al–Hasan bin ar-Rabiy´: Sa´iyd bin ´Abdul-Ghaffaar amenihadithia:
”Nilikuwa mimi na Muhammad bin Yuusuf al-Aswbahaaniy wakati alipofikiwa na barua ya Muhammad bin al-´Alaa bin al-Musayyab kutoka Baswrah. Muhammad bin Yuusuf akaisoma na kunambia: “Je huoni alichoniandikia Muhammad bin al-´Alaa?” Ndani yake mna haya: “Ee ndugu yangu kipenzi! Anayempenda Allaah basi hupenda asijulikane na watu.”
37 – Abu Bakr ash-Shaybaaniy amenihadithia: Nimemsikia Sufyaan bin ´Uyaynah akisema: Bishr bin Mansuur amenambia:
“Hakuna yeyote ambaye ataaibishwa Siku hiyo kiasi kwamba aibu yake ifichikane kwa yeyote.”
38 – Muhammad bin al-Jubayr amenihadithia: ´Abdul-Wahhaab bin ´Atwaa’ amenihadithia, kutoka kwa Sa´iyd, kutoka kwa Qataadah, ambaye amesema:
“Hakuna mtu ataaibishwa Siku hiyo kiasi kwamba aibu yake ifichikane kwa yeyote.”
39 – Ishaaq bin Ibraahiym ametuhadithia: Sufyaan ametuhadithia:
“Nimemwona ath-Thawriy katika usingizi, nikamwambia: ”Niusie.” Akasema: ”Punguza kujulikana na watu.”
40 – Ishaaq bin Ismaa´iyl ametuhadithia: Jariyr ametuhadithia, kutoka kwa Mughiyrah, aliyesimulia kwamba Sammaak bin Salamah amesema:
“Ewe moyo, jihadhari na kuwa na marafiki wengi!”
- Muhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiyd-Dunyaa (afk. 281)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-ul-Khumuul wat-Tawaadhwu´, uk. 55-68
- Imechapishwa: 22/01/2026
30 – Ahmad bin ´Iysaa al-Miswriy amenihadithia: ´Abdullaah bin Wahb ametuhadithia, kutoka kwa ´Amr bin al-Haarith na Ibn Lahiy´ah, kutoka kwa Yaziyd bin Abiy Habiyb, kutoka kwa Sinaan bin Sa´d, kutoka kwa Anas bin Maalik, kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), ambaye amesema:
“Inatosha kuoneysha uovu wa mtu, isipokuwa yule ambaye amekingwa na (´Azza wa Jall), kuwa watu wamuelekezea vidole katika dini yake na dunia yake.”
31 – Ishaaq bin al-Bahluul at-Tanuukhiy ametuhadithia: Ibn Abiy Fudayk ametuhadithia: Muhammad bin Sulaymaan al-Akhnasiy ametuhadithia, kutoka kwa ´Abdul-Waahid bin Abiy Kathiyr, kutoka kwa Jaabir bin ´Abdillaah, ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Inatosha kuoneysha uovu wa mtu, isipokuwa yule ambaye amekingwa na (´Azza wa Jall), kuwa watu wamuelekezea vidole katika dini yake na dunia yake. Hakika Allaah hatazami sura zenu; lakini anazitazama nyoyo na matendo yenu.”
32 – ´Aliy bin al-Ja´d ametuhadithia: al-Mubaarak bin Fadhwaalah ametukhabarisha, kutoka kwa al-Hasan, aliyeeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Inatosha kuoneysha uovu wa mtu watu wanamuelekezea vidole katika dini yake na dunia yake.”
33 – Abun-Naswr al-Mu-addib amenihadithia: Daawuud bin al-Muhabbir ametuhadithia, kutoka kwa al-Mubaarak bin Fadhwaalah, ambaye amesema:
”Tulimwambia al-Hasan: ”Ee Abu Sa´iyd, hakika watu wakikuona wanakuashiria kwa vidole.” Akasema: ”Si hicho kilichokusudiwa hapa. Hakika hapana vyenginevyo kilichoksudiwa ni mzushi katika dini yake na fasiki katika dunia yake.”
34 – Baba yangu amenihadithia: Ibraahiym bin Hiraasah ametuhadithia, kutoka kwa al-Quraah, kutoka kwa mzee mmoja kutoka Ahnaf, ambaye ameeleza kuwa amemsikia ´Aliy akisema:
“Jidunike, acha kujulikana. Usijiinue mwenyewe ukatajwa na hivyo ukatambulika. Kithirisha kukaa kimya utasalimika, wafurahishe wema na wachukize waovu.”
35 – Ahmad bin Ibraahiym ametuhadithia: Ahmad bin Kurduus ametuhadithia: Makhlad bin al-Husayn ametuhadithia, kutoka kwa Abu Bakr bin al-Fadhwl: Nimemsikia Ayyuub akisema:
“Hakuna hatokuwa mkweli na Allaah isipokuwa hufurahi asijulikane mahali alipo.”
36 – Kwa njia hiyohiyo ametuhadithia al-Hasan bin ar-Rabiy´: Sa´iyd bin ´Abdul-Ghaffaar amenihadithia:
”Nilikuwa mimi na Muhammad bin Yuusuf al-Aswbahaaniy wakati alipofikiwa na barua ya Muhammad bin al-´Alaa bin al-Musayyab kutoka Baswrah. Muhammad bin Yuusuf akaisoma na kunambia: “Je huoni alichoniandikia Muhammad bin al-´Alaa?” Ndani yake mna haya: “Ee ndugu yangu kipenzi! Anayempenda Allaah basi hupenda asijulikane na watu.”
37 – Abu Bakr ash-Shaybaaniy amenihadithia: Nimemsikia Sufyaan bin ´Uyaynah akisema: Bishr bin Mansuur amenambia:
“Hakuna yeyote ambaye ataaibishwa Siku hiyo kiasi kwamba aibu yake ifichikane kwa yeyote.”
38 – Muhammad bin al-Jubayr amenihadithia: ´Abdul-Wahhaab bin ´Atwaa’ amenihadithia, kutoka kwa Sa´iyd, kutoka kwa Qataadah, ambaye amesema:
“Hakuna mtu ataaibishwa Siku hiyo kiasi kwamba aibu yake ifichikane kwa yeyote.”
39 – Ishaaq bin Ibraahiym ametuhadithia: Sufyaan ametuhadithia:
“Nimemwona ath-Thawriy katika usingizi, nikamwambia: ”Niusie.” Akasema: ”Punguza kujulikana na watu.”
40 – Ishaaq bin Ismaa´iyl ametuhadithia: Jariyr ametuhadithia, kutoka kwa Mughiyrah, aliyesimulia kwamba Sammaak bin Salamah amesema:
“Ewe moyo, jihadhari na kuwa na marafiki wengi!”
Muhusika: Imaam Abu Bakr ´Abdullaah bin Muhammad bin Abiyd-Dunyaa (afk. 281)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Kitaab-ul-Khumuul wat-Tawaadhwu´, uk. 55-68
Imechapishwa: 22/01/2026
https://firqatunnajia.com/06-yule-anayependwa-zaidi-na-allaah-humfanya-asitambulike/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket