Wanaozungumzishwa kuwa funga inalawazimu kunaingia mkazi na msafiri, mzima na mgonjwa, mwanamke msafi na mwenye hedhi na mwenye nifasi na mwenye kuzimia. Watu wote hawa ni lazima kwao kufunga juu ya dhimma yao kwa njia ya kwamba ndio wanaozungumzishwa kufunga waitakidi ulazima wake katika dhimma yao na kuazimia kutekeleza ima kwa njia ya kuitekeleza mwanzoni au kwa kuilipa baadaye. Wako ambao wanazungumzishwa kufunga katika mwezi huohuo kwa njia ya kuitekeleza. Nao ni wale ambao ni wazima na ni wakazi. Isipokuwa tu ambao wana hedhi na damu ya uzazi. Wako wanaozungumzishwa kwa njia ya kulipa baadaye. Nao ni wale wenye hedhi, wenye damu ya uzazi, mgonjwa anayetakiwa kufunga na anaweza kulipa baadaye. Na wako ambao zinawahusu hali zote mbili. Nao ni msafiri na mgonjwa ambaye anaweza kufunga licha ya uzito usiyokhofiwa kumwangamiza.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Mulakhasw al-Fiqh (01/376)
  • Imechapishwa: 25/03/2021