27 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo mkononi Mwake, lau msingelikuwa mnafanya dhambi basi Allaah angekuondosheni na akaleta watu wengine wanaotenda dhambi na kumuomba Allaah msamaha ambapo akawasamehe.”[1]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Katika Hadiyth hii Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameapa – naye ni mkweli ingawa asingeapa – lakini amefanya hivo ili kutilia mkazo jambo hili. Mara nyingi alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiapa kwa Ambaye nafsi yake imo mkononi Mwake. Hadiyth inafahamisha kuwa Allaah yuko na mkono na wanaraddiwa waliopinga mkono huo. Inafahamisha kuwa nafsi zimo mkononi mwa Allaah. Aidha Hadiyth inafahamisha kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amewakadiria viumbe kutenda dhambi kutokana na ile hekima ambayo Allaah anaijua ya mja kurejea Kwake, kutubia Kwake kutokana na madhambi, kutambua uola wa Allaah na kukiri dhambi aliyofanya.
[1] Muslim (2749).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 31-32
- Imechapishwa: 06/10/2025
27 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo mkononi Mwake, lau msingelikuwa mnafanya dhambi basi Allaah angekuondosheni na akaleta watu wengine wanaotenda dhambi na kumuomba Allaah msamaha ambapo akawasamehe.”[1]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Katika Hadiyth hii Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameapa – naye ni mkweli ingawa asingeapa – lakini amefanya hivo ili kutilia mkazo jambo hili. Mara nyingi alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiapa kwa Ambaye nafsi yake imo mkononi Mwake. Hadiyth inafahamisha kuwa Allaah yuko na mkono na wanaraddiwa waliopinga mkono huo. Inafahamisha kuwa nafsi zimo mkononi mwa Allaah. Aidha Hadiyth inafahamisha kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amewakadiria viumbe kutenda dhambi kutokana na ile hekima ambayo Allaah anaijua ya mja kurejea Kwake, kutubia Kwake kutokana na madhambi, kutambua uola wa Allaah na kukiri dhambi aliyofanya.
[1] Muslim (2749).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 31-32
Imechapishwa: 06/10/2025
https://firqatunnajia.com/06-kuomba-msamaha-baada-ya-kutenda-dhambi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket