Ibn Maajah amesema: ´Aliy bin Muhammad ametuhadithia: Yahyaa bin Aadam ametuhadithia: Zuhayr ametuhadithia, kutoka kwa Abu Ishaaq, kutoka kwa ´Alqamah, kutoka kwa ´Abdullaah, ambaye amesema:
”Hakika tulimuona Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiswali ndani ya viatu na soksi za ngozi.”[1]
Hadiyth imepokelewa pia na Abu Daawuud at-Twayaalisiy (1/84), Ibn Abiy Shaybah (2/416), Ahmad (1/461) na at-Twahaawiy (1/511). Baadhi wametamka wazi kwamba Abu Ishaaq hakumsikia ´Alqamah. al-Buuswayriy amesema:
“Katika cheni ya wapokezi yumo Abu Ishaaq as-Sabiy´iy ambaye alichanganyikiwa mwishoni mwa maisha yake. Kwa mujibu wa Abu Zur´ah alipokea kutoka kwa Zuhayr bin Mu´aawiyah bin Khadiyj ambaye alichanganyikiwa mwishoni mwa maisha yake.”[2]
Hadiyth kwa cheni ya wapokezi hii ni dhaifu, lakini ni sawa kuitumia kwa lengo la kutilia nguvu.
[1] Ibn Maajah (1/330). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh Sunan Ibn Maajah” (858).
[2] Miswbaah-uz-Zujjaah, uk. 125.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: as-Swalaah fiyn-Ni´aal, uk. 9-10
- Imechapishwa: 28/05/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket