45 – Abu Maalik al-Ashja´iy amesimulia kutoka kwa baba yake: “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akimfunza anayesilimu aseme:
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي وَارْحَمْنِي وَاهْدِنِي وَارْزُقْنِي
“Ee Allaah! Nisamehe, nirehemu, niongoze na uniruzuku.”
Imekuja katika upokezi mwingine:
“Alikuwa mtu anaposilimu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anamfunza swalah, kisha anamwamrisha aombe maneno yafuatayo:
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي، وَارْحَمْنِي، وَاهْدِنِي، وَعَافِنِي وَارْزُقْنِي
“ Ee Allaah! Nisamehe, nirehemu, niongoze, nisalimishe na uniruzuku.”
Imekuja katika upokezi mwingine:
“Kwamba amemsikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baada ya kujiliwa na mtu aliyemuuliza: “Ee Mtume wa Allaah! Niseme nini wakati ninapomuomba Mola wangu?” Akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): “Sema:
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي وَارْحَمْنِي، وَعَافِنِي، وَارْزُقْنِي
“Ee Allaah! Nisamehe, nirehemu, nisalimishe na uniruzuku.”
na akikusanya vidole vyake isipokuwa kidole gumba. Hakika mambo haya [manne] yanakukusanyia dunia na Aakhirah yako.”[1]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Hadiyth hii inajulisha fadhilah ya du´aa hii na kwamba inakukusanyia dunia na Aakhirah. Imepokelewa katika “as-Sunan” ya kwamba imesuniwa kuiomba kati ya Sujuud mbili[2].
[1] Muslim (2697).
[2] Sunan ya Abu Daawuud (850).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 51
- Imechapishwa: 13/10/2025
45 – Abu Maalik al-Ashja´iy amesimulia kutoka kwa baba yake: “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akimfunza anayesilimu aseme:
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي وَارْحَمْنِي وَاهْدِنِي وَارْزُقْنِي
“Ee Allaah! Nisamehe, nirehemu, niongoze na uniruzuku.”
Imekuja katika upokezi mwingine:
“Alikuwa mtu anaposilimu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anamfunza swalah, kisha anamwamrisha aombe maneno yafuatayo:
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي، وَارْحَمْنِي، وَاهْدِنِي، وَعَافِنِي وَارْزُقْنِي
“ Ee Allaah! Nisamehe, nirehemu, niongoze, nisalimishe na uniruzuku.”
Imekuja katika upokezi mwingine:
“Kwamba amemsikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baada ya kujiliwa na mtu aliyemuuliza: “Ee Mtume wa Allaah! Niseme nini wakati ninapomuomba Mola wangu?” Akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): “Sema:
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي وَارْحَمْنِي، وَعَافِنِي، وَارْزُقْنِي
“Ee Allaah! Nisamehe, nirehemu, nisalimishe na uniruzuku.”
na akikusanya vidole vyake isipokuwa kidole gumba. Hakika mambo haya [manne] yanakukusanyia dunia na Aakhirah yako.”[1]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Hadiyth hii inajulisha fadhilah ya du´aa hii na kwamba inakukusanyia dunia na Aakhirah. Imepokelewa katika “as-Sunan” ya kwamba imesuniwa kuiomba kati ya Sujuud mbili[2].
[1] Muslim (2697).
[2] Sunan ya Abu Daawuud (850).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 51
Imechapishwa: 13/10/2025
https://firqatunnajia.com/06-duaa-inayokukusanyia-dunia-na-aakhirah-yako/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket