Hadiyth ya tatu
إِلَيْهِ يَصْعَدُ الْكَلِمُ الطَّيِّبُ وَالْعَمَلُ الصَّالِحُ يَرْفَعُهُ
“Kwake Yeye linapanda neno zuri na kitendo chema hukiinua juu.”[1]
19 – Ahmad bin Hibatillaah ametukhabarisha, kutoka kwa ´Abdul-Mu´izz bin Muhammad al-Harawiy: Tamiym bin Abiy Sa´iyd al-Jurjaaniy ametuhadithia: Muhammad bin ´Abdir-Rahmaan al-Kanjaruudhiy ametuhadithia: Abu ´Amr bin Hamdaan ametuhadithia: Abu Ya´laa al-Mawsiliy ametuhadithia: Daawuud bin ´Amr ametuhadithia: Ibn Abiyz-Zinaad ametuhadithia, kutoka kwa al-A´raj, kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia kuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wanapishana kwenu Malaika wa usiku na Malaika wa mchana. Wanakusanyika katika swalah ya Fajr na swalah ya ´Aswr. Halafu hupanda wale waliolala kwenu ambapo Mola wenu Anawauliza – ilihali ni mjuzi zaidi kuliko wao: “Mmewaachaje waja Wangu?” Wanasema: “Tumewaacha na huku wanaswali na tumewaendea na huku wanaswali.”[2]
Kuna maafikiano juu ya usahihi wake.
20 – Allaah (Ta´ala) amesema:
تَعْرُجُ الْمَلائِكَةُ وَالرُّوحُ إِلَيْهِ
“Malaika na Roho [Jibrily] wanapanda Kwake katika siku kiasi chake ni miaka elfu khamsini.”[3]
Kitenzi (يَصْعَدُ) na (تَعْرُجُ) vina maana moja, nayo ni kupanda. Kunaingia vilevile ile safari ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kupanda juu kwa Mola wake, Malaika wa mauti kupanda juu kwa Mola wake baada ya kumpiga Muusa (´alayhis-Salaam) ambapo likatoka jicho lake na roho kupanda juu ya mbingu ambapo yuko Allaah (Ta´ala).
21 – Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakuna mja yeyote muumini anayetoa swadaqah kutoka katika pato zuri – na wala hakuna kinachopanda kwa Allaah isipokuwa kilicho kizuri – isipokuwa Allaah anaiweka kwenye mkono Wake wa kuume na anailea kama anavyolea mmoja wenu kitekli chake ambapo tende inakuwa kama mlima mkubwa.”[4]
22 – Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuhusu Mola wake:
”Mimi Nimejitosheleza kutokana na mshirika. Hakuna chochote katika kujionyesha kinachopanda Kwangu.”
Yote haya ni mapokezi Swahiyh.
23 – Maalik bin Diynaar amesema:
”Nimesoma katika baadhi ya vitabu vilivyoteremshwa kuwa Allaah anasema: ”Ee mwanadamu! Kheri Zangu zinakushukia na shari zako hupanda Kwangu. Wala Malaika mtukufu haachi kupanda Kwangu kutoka kwako akiwa na matendo yako maovu.”
Zipo Hadiyth na mapokezi mengi juu ya maudhui haya.
[1] 35:10
[2] al-Bukhaariy (7429).
[3] 70:4
[4] al-Bukhaariy (7430).
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 46-49
- Imechapishwa: 29/05/2024
Hadiyth ya tatu
إِلَيْهِ يَصْعَدُ الْكَلِمُ الطَّيِّبُ وَالْعَمَلُ الصَّالِحُ يَرْفَعُهُ
“Kwake Yeye linapanda neno zuri na kitendo chema hukiinua juu.”[1]
19 – Ahmad bin Hibatillaah ametukhabarisha, kutoka kwa ´Abdul-Mu´izz bin Muhammad al-Harawiy: Tamiym bin Abiy Sa´iyd al-Jurjaaniy ametuhadithia: Muhammad bin ´Abdir-Rahmaan al-Kanjaruudhiy ametuhadithia: Abu ´Amr bin Hamdaan ametuhadithia: Abu Ya´laa al-Mawsiliy ametuhadithia: Daawuud bin ´Amr ametuhadithia: Ibn Abiyz-Zinaad ametuhadithia, kutoka kwa al-A´raj, kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesimulia kuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wanapishana kwenu Malaika wa usiku na Malaika wa mchana. Wanakusanyika katika swalah ya Fajr na swalah ya ´Aswr. Halafu hupanda wale waliolala kwenu ambapo Mola wenu Anawauliza – ilihali ni mjuzi zaidi kuliko wao: “Mmewaachaje waja Wangu?” Wanasema: “Tumewaacha na huku wanaswali na tumewaendea na huku wanaswali.”[2]
Kuna maafikiano juu ya usahihi wake.
20 – Allaah (Ta´ala) amesema:
تَعْرُجُ الْمَلائِكَةُ وَالرُّوحُ إِلَيْهِ
“Malaika na Roho [Jibrily] wanapanda Kwake katika siku kiasi chake ni miaka elfu khamsini.”[3]
Kitenzi (يَصْعَدُ) na (تَعْرُجُ) vina maana moja, nayo ni kupanda. Kunaingia vilevile ile safari ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kupanda juu kwa Mola wake, Malaika wa mauti kupanda juu kwa Mola wake baada ya kumpiga Muusa (´alayhis-Salaam) ambapo likatoka jicho lake na roho kupanda juu ya mbingu ambapo yuko Allaah (Ta´ala).
21 – Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakuna mja yeyote muumini anayetoa swadaqah kutoka katika pato zuri – na wala hakuna kinachopanda kwa Allaah isipokuwa kilicho kizuri – isipokuwa Allaah anaiweka kwenye mkono Wake wa kuume na anailea kama anavyolea mmoja wenu kitekli chake ambapo tende inakuwa kama mlima mkubwa.”[4]
22 – Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuhusu Mola wake:
”Mimi Nimejitosheleza kutokana na mshirika. Hakuna chochote katika kujionyesha kinachopanda Kwangu.”
Yote haya ni mapokezi Swahiyh.
23 – Maalik bin Diynaar amesema:
”Nimesoma katika baadhi ya vitabu vilivyoteremshwa kuwa Allaah anasema: ”Ee mwanadamu! Kheri Zangu zinakushukia na shari zako hupanda Kwangu. Wala Malaika mtukufu haachi kupanda Kwangu kutoka kwako akiwa na matendo yako maovu.”
Zipo Hadiyth na mapokezi mengi juu ya maudhui haya.
[1] 35:10
[2] al-Bukhaariy (7429).
[3] 70:4
[4] al-Bukhaariy (7430).
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy (afk. 748)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Arba´iyn fiy Swifaati Rabb-il-´Aalamiyn, uk. 46-49
Imechapishwa: 29/05/2024
https://firqatunnajia.com/05-hadiyth-wanapishana-kwenu-malaika-wa-usiku-na-malaika-wa-mchana/