3 – Kusherehekea mazazi ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kujifananisha na wakristo ambao wanasherehekea kuzaliwa kwa Masiyh (´alayhis-Salaam). Kujifananisha na wakristo ni jambo lililoharamishwa vibaya sana. Kumepokelewa Hadiyth zinazokataza kujifananisha na makafiri na maamrisho ya kwenda kinyume nao. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Yeyote mwenye kujifananisha na watu basi yeye ni katika wao.”[1]

Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Jitofautisheni na washirikina.”[2]

Makatazo haya ni khaswa katika yale mambo ambayo yanakumbushia nembo za dini zao.

[1] Ahmad (02/50) na Abu Daawuud (04/314).

[2] Muslim (01/222) (nr. 259).

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Huquwq-un-Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) bayn al-Ijlaal wal-Ikhlaal, uk. 150
  • Imechapishwa: 06/09/2025