4- ´Aliy bin Hamshaad (kfrk. 338) tabaka 11
adh-Dhahabiy ameandika wasifu wake katika “at-Tadhkirat-ul-Huffaadhw” na akasema:
“Haafidhw mkubwa Abul-Hasan an-Naysaabuuriy, mtunzi wa tungo nyingi. Alisikia kutoka kwa al-Husayn bin al-Fadhwl, al-Fadhwl ash-Sha´raaniy, al-Haarith bin Abiy Usaamah, Ibraahiym bin Dayziyl, Ismaa-iyl al-Qaadhwiy na wengineo.
al-Haakim amesikia kutoka kwake, akamsifu na akamuadhimisha kwa hali ya juu. Kitabu chake “al-Musnad” kina juzu 400, “al-Ahkaam” yake ina juzu 260 na tafsiri yake ya Qur-aan ina mijeledi kumi.
Abu Ahmad al-Haakim amepokea kutoka kwake na akasema:
“Sijawahi kumuona yeyote katika wanachuoni wetu ambaye ni thabiti zaidi kama yeye.”
Mtoto wake amesema:
“Sijui kama kuna siku yoyote baba yangu aliacha swalah ya usiku.”
Alifariki katika Shawwaal mwaka wa 338. Allaah amrehemu.
- Muhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tadhkiyr-un-Naabihiyn, uk. 38-39
- Imechapishwa: 10/06/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)