04. Hadiyth “Yeyote mwenye kuja katika msikiti huu… “

87- Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) kwamba amemsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:

“Yeyote mwenye kuja katika msikiti huu na hakuja kwa jengine isipokuwa ima ajifunze au afunze jambo la kheri, basi yuko katika daraja  ya mpambanaji katika njia ya Allaah. Na yeyote mwenye kuja kwa jambo jengine basi yuko katika daraja ya mtu anayetazama mali za wengine.”[1]

Ameipokea Ibn Maajah na al-Bayhaqiy. Hakuna katika cheni ya wapokezi ambaye ameachwa au ambaye kuna maafikiano juu ya unyonge wake.

[1] Swahiyh.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/146)
  • Imechapishwa: 01/05/2020
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy