141- Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hawakupotea watu baada ya uongofu walikuwemo isipokuwa kulianza ubishi kwanza:
Kisha Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasoma Aayah isemayo:
مَا ضَرَبُوهُ لَكَ إِلَّا جَدَلًا ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ خَصِمُونَ
”Hawakukupigia mfano huo isipokuwa tu kutaka kubisha. Bali wao ni watu mahasimu.”[1][2]
Ameipokea at-Tirmidhiy, Ibn Maajah na Ibn Abiyd-Dunyaa katika ”Kitaab-us-Swamt” na wengineo. at-Tirmidhiy amesema:
“Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.”[3]
[1] 43:58
[2] Nzuri.
[3] al-Haakim pia ameisahihisha na ad-Dhahabiy akaafikiana naye. Hata hivyo ni nzuri tu.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/169-170)
- Imechapishwa: 07/05/2020
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)