04. Hadiyth ”Babu yangu, Aws, wakati mwingine alikuwa akiswali… ”

Ibn Maajah (1/330) amesema: Abu Bakr bin Abiy Shaybah ametuhadithia: Ghundar ametuhadithia, kutoka kwa Shu´bah, kutoka kwa an-Nu´maan bin Saalim, kutoka kwa Ibn Abiy Aws, ambaye ameeleza:

”Babu yangu, Aws, wakati mwingine alikuwa akiswali na alikuwa akinionyesha kwa ishara akiwa ndani ya swalah kwamba nimpe viatu vyake. Kisha akasema: ”Nilimuona Mtume wa Allaah  (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiswali akiwa amevaa viatu vyake.”

Ameipokea Ibn Abiy Shaybah (2/415), at-Twahaawiy (1/512) na Ahmad (4/8-10).

al-Buuswayriy amesema:

“Cheni yake ya wapokezi ni Swahiyh.” [1]

al-Haythamiy amesema:

“Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Mu´jam al-Kabiyr”. Wasimulizi wake ni wenye kuaminika.”[2]

[1] Miswbaah-uz-Zujaajah, uk. 125.

[2] Majma´-uz-Zawaa’id (2/55).

  • Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: as-Swalaah fiyn-Ni´aal, uk. 7
  • Imechapishwa: 28/05/2025