16 – Abu Khaythamah ametuhadithia: Jariyr ametuhadithia, kutoka kwa al-A´mash, kutoka kwa Maalik bin al-Haarith, kutoka kwa Abu Khaalid, Shaykh mmoja katika maswahiba zake ´Abdullaah, aliyesema:

”Wakati tulipokuwa msikitini alikuja Khabbaab bin al-Aratt akaketi chini. Akanyamaza. Ndipo watu wakamwambia: ”Maswahiba zako wamekukusanyikia uwazungumzishe au kuwaamrisha jambo.” Akasema: ”Niwaamrishe kitu gani? Huenda nikawaamrisha jambo ambalo mimi silifanyi.”

17 – Abu Khaythamah ametuhadithia: Wakiy´ ametuhadithia: Abu Sinaan Sa´iyd bin Sinaan ametuhadithia: ´Antarah amenihadithia: Nimemsikia Ibn ´Abbaas akisema:

”Mtu hatoshika njia akitafuta kwayo elimu, isipokuwa Allaah humsahilishia kwayo njia ya kuelekea Peoni.”[1]

18 – Abu Khaythamah ametuhadithia: Wakiy´ ametuhadithia, kutoka kwa Mis´ar, kutoka kwa Ma´n bin ´Abdir-Rahmaan: ´Abdullaah amesema:

”Ukiweza wewe kuwa ndiye mwenye kuzungumza, basi fanya hivo.”

19 – Abu Khaythamah ametuhadithia: Wakiy´ ametuhadithia, kutoka kwa Sufyaan bin ´Uyaynah, kutoka kwa ´Amr, kutoka kwa Yahyaa bin Ja´dah, ambaye amesema:

”Watu walikuwa wakimjia Salmaan kusikiliza maneno yake. Akasema: ”Haya ni kheri kwenu na ni shari kwangu.”

20 – ´Abdullaah ametuhadithia: Abu Khaythamah ametuhadithia: Sufyaan bin ´Uyaynah ametuhadithia, kutoka kwa Yuunus, kutoka kwa al-Hasan, ambaye amesema:

”Wakati hutokea mtu akakaa kwenye kikao ambapo watu wakamuona kuwa si mjuzi. Si kwamba sio mjuzi; ni mwanachuoni muislamu.”

21 – Abu Khaythamah ametuhadithia: Jariyr ametuhadithia, kutoka kwa ´Atwaa’ bin as-Saa-ib, kutoka kwa ´Abdur-Rahmaan bin Abiy Laylaa, aliyesema:

”Nilikutana na Maswahabah mia na ishirini wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Wanusuraji. Hakuna yeyote katika wao ambaye anaulizwa jambo isipokuwa alitamani badala yake ndugu yake alijibu. Hakuna yeyote katika wao aliyezungumzia jambo isipokuwa alitamani badala yake ndugu yake ndiye alizungumze.”

22 – Abu Khaythamah ametuhadithia: Sufyaan ametuhadithia, kutoka kwa az-Zuhriy, aliyesema:

”´Urwah alikuwa akiwafanya watu wasikilize mazungumzo yake.”

23 – Abu Khaythamah ametuhadithia: Sufyaan ametuhadithia: ´Amr amesema:

”Wakati ´Urwah alipofika Makkah, alisema: ”Njooni msome kwangu.”

24 – Abu Khaythamah ametuhadithia: Mu´aawiyah bin ´Amr ametuhadithia: Zaa-idah ametuhadithia, kutoka kwa al-A´mash, kutoka kwa Maalik bin al-Haarith, kutoka kwa ´Abdur-Rahmaan bin Yaziyd, ambaye amesema:

”Kulisemwa kuambiwa ´Alqamah: ”Ni kwa nini hukai msikitini, watu wakakukusanyikia na ukaulizwa maswali na sisi tukaketi pamoja nawe? Kwani watu walio chini yako kiujuzi ndio wanaotakiwa kuulizwa.” ´Alqamah akasema: ”Nachukia visigino vyangu vikakanyagwa na ikasemwa: “Huyu ni Alqamah! Huyu ni ‘Alqamah!”

[1] Cheni ya wapokezi ni nzuri. Muslim na wengine wamepokea mfano wake kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kupitia kwa Abu Hurayrah. Itakuja huko mbele ya kitabu (25).

  • Mhusika: Imaam Abu Khaythamah Zuhayr bin Harb an-Nasaa’iy (afk. 234)
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-ul-´Ilm, uk. 10-13
  • Imechapishwa: 12/06/2024
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy