122- Abu Hurayrah amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mfano wa ambaye amejifunza elimu kisha asiizungumzie ni kama mfano wa ambaye anarundika hazina lakini hatoi kutoka katika hazina hiyo.”[1]
Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Awsatw”. Katika cheni ya wapokezi yuko Ibn Lahiy´ah[2].
[1] Nzuri na Swahiyh.
[2] Bi maana ni dhaifu. Lakini ni katika upokezi wa Ibn Wahb, kutoka kwa Ibn Lahiy´ah, kutoka kwa Darraaj Abus-Samh, kutoka kwa Abul-Haytham na ´Abdur-Rahmaan bin Hujayrah, kutoka kwa Abu Hurayrah. Cheni ya wapokezi ni nzuri kwa sababu masimulizi ya Ibn Lahiy´ah kutoka kwa Ibn Wahb ni Swahiyh. Pia masimulizi ya Darraaj ni Hadiyth nzuri kutoka kwa Ibn Hujayrah. Aidha Hadiyth hii ina njia nyenginezo na shawahidi zinazoipa nguvu. Nimeitaja katika ”as-Swahiyhah” (3479).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/160)
- Imechapishwa: 05/05/2020
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
122- Abu Hurayrah amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mfano wa ambaye amejifunza elimu kisha asiizungumzie ni kama mfano wa ambaye anarundika hazina lakini hatoi kutoka katika hazina hiyo.”[1]
Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Awsatw”. Katika cheni ya wapokezi yuko Ibn Lahiy´ah[2].
[1] Nzuri na Swahiyh.
[2] Bi maana ni dhaifu. Lakini ni katika upokezi wa Ibn Wahb, kutoka kwa Ibn Lahiy´ah, kutoka kwa Darraaj Abus-Samh, kutoka kwa Abul-Haytham na ´Abdur-Rahmaan bin Hujayrah, kutoka kwa Abu Hurayrah. Cheni ya wapokezi ni nzuri kwa sababu masimulizi ya Ibn Lahiy´ah kutoka kwa Ibn Wahb ni Swahiyh. Pia masimulizi ya Darraaj ni Hadiyth nzuri kutoka kwa Ibn Hujayrah. Aidha Hadiyth hii ina njia nyenginezo na shawahidi zinazoipa nguvu. Nimeitaja katika ”as-Swahiyhah” (3479).
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/160)
Imechapishwa: 05/05/2020
Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/03-hadiyth-mfano-wa-ambaye-amejifunza-elimu/