Je, talaka inakuwa mkononi mwa mwanamke au mwanaume? Kimsingi ni kwamba talaka inakuwa mkononi mwa mwanamme kwa mujibu wa dalili ya Qur-aan na Sunnah. Amesema (Ta´ala):
لَّا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ إِن طَلَّقْتُمُ النِّسَاءَ مَا لَمْ تَمَسُّوهُنَّ أَوْ تَفْرِضُوا لَهُنَّ فَرِيضَةً
”Hapana dhambi kwenu mkiwataliki wanawake ambao hamkuwagusa au kuwawekea wazi mahari yao.”[1]
وَإِنْ أَرَدتُّمُ اسْتِبْدَالَ زَوْجٍ مَّكَانَ زَوْجٍ وَآتَيْتُمْ إِحْدَاهُنَّ قِنطَارًا
“Mkitaka kubadlisha mke mahali pa mke na mkampa mmoja wao [zawadi ya] mirundi ya mali.”[2]
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نَكَحْتُمُ الْمُؤْمِنَاتِ ثُمَّ طَلَّقْتُمُو
“Enyi walioamini! Mnapofunga ndoa na waumini wa kike kisha mkawataliki… ”[3]
يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ إِذَا طَلَّقْتُمُ النِّسَاءَ فَطَلِّقُوهُنَّ لِعِدَّتِهِنَّ
“Ee Nabii! Mtakapowataliki wanawake, basi watalikini katika wakati wa twahara zao.”[4]
Imekuja katika Hadiyth kupitia kwa Ibn ´Umar ambaye amesema:
”Nilimuoa mwanamke niliyempenda na baba yangu alikuwa akimchukia. Ndipo baba yangu akaniamrisha kumtaliki ambapo nikakataa. Baadaye nikamtajia hilo Mtume ambaye alisema: ”Ee ´Abdullaah mwana wa ´Umar, mwache mwanamke wako!”[5]
Ameipokea at-Tirmidhiy ambaye amesema kuwa Hadiyth ni nzuri na Swahiyh. Ameipokea al-Haakim pia naye pia akaisahihisha.
Imepokelewa kutoka kwa Ibn ´Umar pia kwamba alimtaliki mke wake hali ya kuwa na hedhi. ´Umar akamweleza hilo Mtume ambapo akasema:
”Mwamrishe amrejee, kisha amtaliki akiwa amesafika au mjamzito.”[6]
Ameipokea Ibn Maajah (2023).
Mwanamke wa Qays bin Shammaas ambaye amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia:
”Kubali shamba kisha umtaliki.”[7]
Tutataja maana ya Hadiyth katika masuala mengine kwa ukamilifu wake.
[1] 02:236
[2] 04:20
[3] 33:49
[4] 65:01
[5] at-Tirmidhiy (04/169) (7653), al-Haakim katika ”al-Mustadrak” (7653). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Ibn Maajah (2088).
[6] Ibn Maajah (2023). Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Ibn Maajah (1643).
[7] al-Bukhaariy (5673).
- Muhusika: Shaykh Jamaal bin Furahyaan al-Haarithiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Twalaaq – asbaabuhu wa ´ilaajuh, uk. 16-17
- Imechapishwa: 26/03/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)